MTANGAZAJI

MARA:KITUO CHA SHERIA NA HAKI ZA BINADAMU KUTOA MSAADA WA KISHERIA KWA WIKI NZIMA WILAYANI SERENGETI



Kituo cha sheria na haki za binadamu kupitia mawakili na wana sheria wake kwa kushirikiana na wasaidizi wa kisheria na haki za binadamu wilayani Serengeti mkoani Mara wameanza wiki ya msaada wa kisheria bure kwa wakazi wa wilaya hiyo.

Mwanasheria kutoka kituo hicho Rodrick Kimaro amesema lengo nikutoa msaada wa kisheria bure kwa jamii kuhusiana  na maswala ya kisheria, ushauri,na kuwajengea uwezo wasaidizi wa kisheria na haki za binadamu kuwasaidia wananchi wasio na uwezo wakupata haki.

Aidha wananchi wenye matatizo mbalimbali ya kisheria wilayani Serengeti,wajitokeze julai 5 mwaka huu ili waweze kupewa msaada wa kisheria na ushauri.

Mwenye kiti wa shirika la wasaidizi wa kisheria na haki za binadamu wilayani Serengeti Samuel Mewama amesema huduma hiyo ambayo imekuwa ikitolewa kila mwaka imesaidia wananchi kujua haki zao na kuzidai na hivyo kuimarisha utawala bora. Katika zoezi kama hilo  mwaka jana migogoro mingi ulihusu miradhi,ukatili  wa kijinsia,migogoro ya ardhi na ndoa.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.