MTANGAZAJI

VIJANA 25 WA KITANZANIA WAHUKUMIWA ADHABU YA KIFO CHINA



Takribani vijana 65 wa Kitanzania wamehukumiwa adhabu ya kifo huko nchini China baada ya kupatikana  na hatia ya kujihusisha na dawa za kulevya.


Vijana hao ni kati ya zaidi ya 403 wa Tanzania wanaoshikiliwa katika nchi mbalimbali duniani kwa tuhuma ya kujihusisha na biashara hizo.


Hayo yamesemwa hapo jana na Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu(sera utaratibu na Bunge)William Lukuvi,mjini Dodoma wakati akizungumzia maadhimisho ya siku ya Dawa za kulevya Duniani yanayofanyika juni 26 kila mwaka.


Lukuvi amesema kuwa kwa mwaka huu maadhimisho  ya kesho,kitaifa yatafanyika katika viwanja vya shule ya msingi Nzovwe jijini Mbeya na Makamu wa Rais,Dk Gharib Bilal,anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.


Amezitaja baadhi nchi ambako vijana wanashikiliwa kuwa ni Brazil(108),Hong kong (118),Kenya(34),Pakistan(16)na China 65.






No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.