MTANGAZAJI

WAKUU WA MIKOA YA SHINYANGA NA TABORA WAUNDA TUME YA KUCHUNGUZA MGOGORO WA ARDHI



Wakuu wa Mikoa ya Shinyanga na Tabora wameunda tume ya watu 18 kuchunguza chanzo cha mgogoro wa ardhi kati ya wakulima na wafugaji wa wilaya za kishapu mkoani shinyanga na Igunga mkoani Tabora.

Hatua hiyo inafuatia ugomvi wa mipaka uliosababisha vifo vya watu watano na imeazimiwa katika kamati ya ulinzi na usalama za mikoa hiyo kilichofanyika katika kijiji cha Magogo ambapo vurugu hizo zimetokea.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bwana Ali Lufunga na  mkoa wa Tabora Bi Fatuma Mwasa wamesema kikao hicho kimeazimia kuwa wafugaji walioko katika kijiji cha Magalata wilayani Kishapu wabakie kwenye eneo lao na wasivuke mto Manonga kulisha Ng’ombe wao,huku wakulima walioko katika vijiji vya Magogo na IsakaMaliwa wilaya ya Igunga mkoani Tabora  wasivuke Mto Manonga.

Aidha wakulima walioharibiwa makazi  katika vijiji vya Magogo na IsakaMaliwa wametakiwa kuendelea na shughuli zao wakati serikali ikiimarisha ulinzi kwa kuongeza askari polisi pamoja na kuwatafuta walioharibu makazi yao.

Kwa pamoja wakuu hao wa mikoa wamelaani vitendo vilivyofanywa na wafugaji wa jamii ya kithatulu na kusema ni vitendo visivyovumilika.

Chanzo:Radio Free Afrika

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.