MTANGAZAJI

MKUTANO WA UWAKILI WA KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO WAENDELEA KATIKA KANDA YA KASKAZINI MASHARIKI MWA TANZANIA



Mkutano wa idara ya uwakili ya Kanisa la Waadventista Wa Sabato unaendelea kwa takribani siku saba ukihusisha viongozi mbalimbali na washiriki wa makanisa. 

Mkutano huo unaoendelea katika makanisa mbalimbali ya Waadventista Wa Sabato jimbo la kaskazini mashariki mwa Tanzania[ NETC] ni kwa ajili ya kuwainua washiriki katika  kiroho,kuwa na malengo mazuri katika utoaji pamoja na kujenga uhusiano bora wa ndoa,namna ya kuhusiana kwa karibu na Mungu lakini pia kuhakikisha uhusiano na jamii unakuwa mzuri.

 Akihutubia waumini na wageni walioalikwa katika kanisa la waadventista wasabato mtaa wa mbauda jijini Arusha mapema wiki hii mchungaji Julius Mbwambo kutoka chuo kikuu cha Bugema nchini Uganda ameeleza kuwa uwakili wa mkristo sio tukio la siku moja linalokuja na kupita bali ni swala endelevu ambalo huwa mtindo wa maisha ya mwanadamu katika kumwakilisha Mungu Duniani.

 Mahudhurio ya mkutano huo katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato mtaa wa Mbauda zaidi ya watu mia mbili kwa siku tangia ulipoanza siku ya jumamosi mchana.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.