MTANGAZAJI

SERIKALI YA TANZANIA YAFUTIA USAJILI SHIRIKA LISILO LA KISERIKALI

Serikali ya Tanzania imefutilia mbali usajili wa shirika moja lisilokuwa la kiserikali kwa sababu ya kuhamasisha mapenzi ya jinsia moja katika jamii.

Shirika hilo kwa jina Sisi Kwa Sisi lilisajiliwa baada ya kudai kuwa malengo yake yalikuwa ni kusaidia jamii.


Tanzania imesema imechukua hatua ya kufutilia mbali usajili wa shirika hilo kwa kukiuka sheria za nchi na kwenda kinyume na malengo ya usajili wake.


Mkurugenzi wa usajili wa mashirika yasiyo ya Kiserikali nchini Tanzania, Maseli Katemba, amesema kuwa shirika hilo la Sisi kwa Sisi limekiuka malengo yake ya awali ya kuwapa elimu na misaada ya kifedha wananchi lakini mambo yakawa tofauti..


Bwana Katemba amesema kuwa Serikali itaendelea na kuyasaka makundi mengine kama hayo ambayo yanaendesha maswala yaliyo kinyume na sheria za Tanzania.

Chanzo:BBC

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.