MTANGAZAJI

JAMII YATAKIWA KUJENGA MAZOEA YA KUCHUNGUZA AFYA



Jamii ya kitanzania imetakiwa kujenga mazoea na desturi ya kuchunguza afya zao kabla ya kusubiri kuumwa.

Hayo yamezungumzwa wakati ambapo Jumla ya madakitari kumi kutoka chama cha madakitari wanawake Tanzania {Mewata}wakati wa zoezi la kupima afya lililofanyika bure mapema jana kwa jamii hususani ugonjwa wa saratani ya matiti,kisukari na shinikizo la damu katika kanisa la waadventista wasabato Njiro.

Akizungumza na wanahabari Mkurugenzi wa huduma ya afya na kiasi wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato Njiro Dr. Peter Mabula amesema  zoezi limefanikiwa kwa kiwango kikubwa na zaidi ya wanawake mia moja wamefanyiwa uchunguzi wa saratani ya matiti,kisukari na shinikizo la damu kati yao wachache wameonekana na viashiria vya magonjwa hayo hivyo idara ya afya na kiasi ya kanisa  kwa kushirikiana na chama cha madakitari wanawake{ MEWATA}pamoja na wadau wengine wa afya wanafanya mpango wa kuwapatia huduma ya matibabu wale wote walioonekana na viashiria hivyo.

Hata hivyo wananchi waliojitokeza katika zoezi hilo muhimu wameipongeza idara ya afya na kiasi ya Kanisa la Waadventista Wa Sabato Njiro, kwa kuratibu na kuandaa mpango huo ambao wameuita ni msaada wa karibu kwa jamii ya mwanamke Mtanzania. hivyo wameomba elimu itolewe pia kwa wanaume kujua na kutambua kuwa, hata wao wanaweza kupatikana na ugonjwa wa saratani ya matii, hivyo wajitokeze kuchunguza afya zao ili kupatiwa huduma mapema.

Na Abel Kinyongo

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.