MTANGAZAJI

UTAFITI:NYANYASAJI WA KINGONO BADO NI TATIZO NCHINI TANZANIA



Utafiti wa uliofanywa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu nchini Tanzania (LHCR) na kuutoa katika ripoti yake ya Haki za Binadamu na Biashara ya Mwaka 2013 umegundua kuwa kwa upande wa haki za kinjinsia,unyanyasaji wa kingono umefikia asilimia 28.3 nchini Tanzania.

Japokuwa unyanyasaji wa kijinsia makazini unaonekana kupungua kutokana na kuongezeka kwa ufahamu wa haki za Binadamu bado ukandamizaji wa namna mbalimbali umefikia asilimia 49 na asilimia 10 ya wafanyakazi wa kike katika makampuni ndio waliopewa likizo ya uzazi.

Ripoti hiyo iliyotolewa mapema juma hili jijini Dar es salaam imetokana na utafiti kwenye mikoa 15 ya Tanzania bara ambapo watafiti 30 walihusika katika kukusanya takwimu mbalimbali toka kwa watu zaidi ya 1,000 ,makampuni 153 na ofisi 121 za serikali zilitoa taarifa mbalimbali.

Maeneo yaliyohusika na ripoti hiyo ni Haki za Ajira,Haki za Ardhi,Kodi,Uwajibikaji wa Makampuni kwa Jamii na Serikali,Haki za Mazingira na Haki za Kijinsia.

Ripoti hiyo imeeleza kuwa ni sehemu ya mpango mkakati wa LHCR mwaka 2013 hadi 2018 katika kufuatilia uwajibikaji wa makampuni kwa viwango vya ndani na vya kimataifa kwenye haki za kiuchumi,kijamii na mazingira.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.