MTANGAZAJI

MAKANISA YA WAADVENTISTA WASABATO ARUSHA WAENDESHA HUDUMA ZA KIJAMII NA KIROHO KATIKA GEREZA

Zaidi  ya watoto 30 katika Gereza la watoto lijulikanalo kwa jina la Home Center lililoko Unga Ltd Arusha wanapata mafunzo ya kiroho kutoka kwa wainjilisti na Idara ya Dorkasi ya kanisa la Waadventista Wa Sabato Njiro jijini Arusha.
 
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa Muinjilisti Gerald Nyafanga  wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato Njiro anayeendesha masomo na maombi  katika Gereza hilo amemwambia mwandishi wa habari hii asubuhi ya leo  kuwa kuna umuhimu wa kuongeza nguvu zaidi ya huduma za kiroho katika kitengo hicho na vingine vinavyofanana na hivyo ili kuikoa jamii na matendo mabaya lakini pia kuifanya jamii ya watu hao kuwa na amani pia tumaini juu ya Mungu.
 
Zaidi ya maombi na mafunzo hayo watoto hao pia hupata misaada mbalimbali kutoka kwa kanisa hilo ikiwa ni pamoja na vyakula,sabuni, mafuta,pia wanapata nafasi ya kufanya mijadala mbalimbali ihusuyo Biblia,madhara ya madawa ya kulevya,ubaya wa uhalifu kwa Mungu na kwa jamii inayozunguka.

Kanisa hilo pia limeanzisha darasa la muziki katika Gereza hilo darasa ambalo lina ongozwa na kiongozi wa muziki wa Kanisa hilo la Waadventista Wa Sabato Njiro.

Mbali na hayo wafungwa pamoja na viongozi wa gereza hilo la watoto wameonyesha kuyapenda mafunzo  na wameeleza kuwa yatakuwa ni msaada   mkubwa na chachu  katka kuitengeneza jamii hiyo iweze kubadili mwelekeo uliokuwa mbaya na kumwelekea mungu wa mbinguni hasa wanapoendesha mijadala kuhusu namna ya kuacha madawa ya kulevya kwani ndilo tatizo kubwa kwa sasa linalowakabili vijana llikiwemo la ulevi, na  ngono.

Mafunzo hayo hufanyika kila siku ya jumatano ya kila juma.


Na.Abel Kinyongo

1 comment

Anonymous said...

Mungu awabariki sana wote wanaofanya huduma hiyo awalinde awatie nguvu na jina la bwana likapate kuinuliwa.

Mtazamo News . Powered by Blogger.