MTANGAZAJI

MWENYEKITI WA KIJIJI ATAKA KUJIUZULU KWA SABABU YA MWEKEZAJI

Mgogoro wa shamba unaoendelea kati ya mmiliki mwenye asili ya kiasia Pradeepo Lodhia  wa shamba la Tanzania Plantation  na wananchi wa kijiji cha Msitu wa Mbogo kata ya Mbuguni wilayani Arumeru mkoani Arusha  umechukua sura mpya baada ya mwenyekiti wa kijiji hicho Ernesti Mkilanya kutangaza kujiuzulu wadhifa wake iwapo wananchi wanaoendelea na uvamizi katika shamba la mwekezaji huyo hawataacha mara moja.

Mwenyekiti wa kijiji huyo ameyasema hayo mapema wiki hii wakati akizungumza na wananchi wa kijiji hicho na kuwataka wananchi kuwataja na kuwafichua  wote wanaohusika kwa njia yoyote ile kuhujumu shamba la mwekezaji huyo mara moja.
 
 Mwenyekiti huyo ameyasema hayo wakati mgogoro huo ukiwa umedumu kwa takribani miezi mitatu sasa
 
 Wito huo umekuja wakati viongozi wa kijiji hicho wakiwa wamepokea barua ya onyo ya kumbukumbu namba 201 ESM inayotoka kwa wakili wa mwekezaji huyo Loamu Ojari inayotaka viongozi wa kijiji hicho wasitishe uvamizi na uharibifu wa mali katika shamba hilo vinginevyo watashitakiwa.
 
Hivyo Bwana Mkilanya amesema atajiuzulu ili kupisha wengine kugombea nafasi hiyo kwani hawezi kushitakiwa mahakamani kwa tuhuma za uvamizi wa shamba hilo wakati yeye pamoja na viongozi wengine wa kijiji hawahusiki na chochote.
 
Aidha bwana Mkilanya alisema kuwa kamati ya ardhi yenye wajumbe 25 iliundwa february 5 mwaka huu na imeshafikisha malalamiko hayo kwa mkuu wa wilaya ya Arumeru ambapo ameahidi kulishughulikia.  
 
Na:Abeli Kinyongo                                                                                                               

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.