MTANGAZAJI

MABANGO YA MORNING STAR TV YAGOMBANIWA

Timu ya Morning Star Television imejikuta ikiingia katika wakati mgumu  pale umati mkubwa ulipowazunguka ukihitaji mabango ya MSTV.  Hili limetokea mara tu baada ya uhamasishaji juu ya kuchangia uanzishaji wa kituo hicho cha Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania, uliofanyika katika Kongamano la viongozi wa kanisa Jijini Mwanza.

Wanasemina wote wengi wakiwa ni wachungaji, watendakazi wa na wazee wa kanisa toka South Nyanza Conference(SNC), Mara Conference , (MC) na Western Tanzania Field(WTF) walipokea taarifa hii kwa furaha na kuahidi kutoa ushirikiano katika kuhamasisha uchangiaji.

Kanisa hilo nchini  Tanzania limeitenga March 2 ,2013 kuwa siku maalum kuchangia TV ya kanisa itakayoanza juni 2013. Studio za Televisheni hiyo ziko Mikocheni B,jijini Dar es salaam,ambapo mchakato wa uandaaji wa vipindi umeshaanza

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.