MTANGAZAJI

MCH.LISSO AZIKWA LEO

Wachungaji waliiongoza ibada ya kumuuaga mwili wa Marehemu Mch Thomas Rukiko Lisso kutoka kushoto Mch. Alex Juma,Mch Lusingu toka Arusha ,Mch Magesa Bina toka Nairobi Kenya,Mch Elias Kasika katibu ETC na Mhazini ETC Ndugu Zablon Masele
Mke wa Marehemu Zebida Lisso(mwenye nguo nyeusi)akiwa na watoto,wajukuu na vituu katika ibada ya kuuga mwili wa Marehemu mumewe

Baadhi ya wachungaji walisoma na kufanya kazi na Marehemu Liso,Mchungaji Manento,Mchungaji Mwasumbi,Mzee Kitalima,Mama Mch.Onyango na Mchungaji Shemu Onyango aliyesoma pamoja na Liso huko Bugema nchini Uganda,ambapo Onyango alikuwa kidato cha kwanza,Liso akiwa kidato cha tatu ambapo alikuwa anafundisha somo la kiswahili kidato cha tatu na cha nne.Hii ni kwa mujibu wa maelezo yalitolewa na Onyango kwa blog hii


Mwinjilisti wa Kimataifa Amon Mkangala na baadhi ya waheshimiwa nao walikuwepo


Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kanisa la Waadventista Wasabato Kanda ya Mashariki mwa Tanzania alijadili jambo na Mkurugezi wa Mawasiliano wa Kanisa hilo katika nchi za Afrika Mashariki na Kati Mch.Magesa Bina kabla ya kuanza kwa ibada ya kuuga mwili wa Marehemu katika kanisa la Waadventista Wasabato Misufini,Morogoro


Mke wa Marehemu akisikiliza hotuba ya kuuaga mwili wa Marehemu ilitolewa na Mch Steven Bina toka makao makuu ya kanisa la Waadventista Wasabato Afrika Mashariki na Kati,Nairobi Kenya




Mbunge wa Musoma Vijijini Mhemshimiwa Nimrodi Mkono alikuwepo,Mzee Liso alishawahi kuwa Mbunge wa jimbo hilo miaka ya 1970


Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Issa Machibya(kushoto) naye alikuwepo

Kwaya ya Mashahidi na Misufini ziliimba wimbo wa pamoja kwa ajili ya kutoa faraja

Baadhi ya wajuu wa marehemu waliunda kundi la Acappela na kumtukuza Mungu kwa wimbo wa matumaini uliogusa watu waliohudhuria tukio hili


Mdogo wake na Marehemu


Mdogo wake na Marehemu akipita mbele ya jeneza kuuga mwili

Baadhi ya ndugu wa Marehemu wakiuaga mwili wa marehemu


Mtoto wa kwanza wa Marehemu Jared Liso akiuaga mwili wa Marehemu



Mke wa Marehemu akiuaga mwili wa marehemu



Mke wa Marehemu Liso akisaidiwa na miongoni mwa waombolezaji baada ya kuuona mwili wa marehemu

Mchungaji Thomas Rujiko Lisso aliyefariki Mei 20,2009 katika hospitali ya mkoa wa Morogoro kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa Malaria,UTI na Numonia amezikwa leo katika makaburi yaliyoko katika viwanja vya makao makuu ya kanisa la Waadventista Wasabato Kanda ya Mashariki mwa Tanzania(ETC).
Alizaliwa Oktoba 1,1921 katika familia ya Ibrahimu Lisso Chabhula Chikwara na Elizabeth Nyakwesi Machumu,alianza maisha ya kifamilia Novemba 24,1942 kwa kufunga pingu za maisha na Zebida Nyamambara Karilo akiwa na miaka 21 na binti miaka 12 na kufanikiwa kupata watoto 11 na waliohai ni 7 ambao ni Jaredi(Kamoga),Tumaini,Ellen,Rose,Margaret,Maiga, na Dorah.
Mara nyingi marehemu alipokuwa akiwapa ushauri watoto wake wakati wa uhai wake katika suala la changamoto za maisha aliwaambia "DONT QUIT FIGHT WITHIN".
Marehemu aliyeacha watoto 7,wajukuu 31 na vituu 9 baada ya kumaliza elimu yake ya shahada ya kwanza katika chuo cha Solusi nchini Zimbabwe amewahi kuwa Mbunge wa jimbo la Musoma vijijini na pia amekuwa mchungaji kwa muda usiopungua miaka 38 akiwaamewahi kuwa mwalimu katika shule za Bugema,Suji,Bwasi,Kibumai na Ikizu hapa nchini na pia aliwahi kuwa Mtafsiri na mhariri wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania.
LALA BABA TUONANE ASUBIHI NJEMA

2 comments

Anonymous said...

Watoto saba, mbona Jared umemsahau au ana majina mawili?

Asante kwa habari.

Mwanaisha Mkangara said...

Mungu aiweke mahala pema peponi roho ya babu yetu mpendwa. Amen

Mtazamo News . Powered by Blogger.