MTANGAZAJI

KIWANGO CHA UTOAJI MIMBA CHAONGEZEKA MAREKANI

 


Zaidi ya mimba 930,000 zilitolewa  nchini Marekani mwaka wa 2020, ikiwa  ongezeko katika kipindi cha mwanzoni mwa  miaka mitatu  kwa mujibu wa  shirika la utafiti linalojihusisha na utafiti wa Uzazi uliopangwa.
Taasisi ya Guttmacher imetoa  data zake za utoaji mimba kwa 2020 juma lililopita, ikiripoti kwamba zaidi ya mimba 930,000 zilitolewa  nchini Marekani  mnamo mwaka 2020, ambalo ni  ongezeko la 8% kutoka utoaji wa mimba 862,320 mnamo mwaka 2017.
Zaidi ya hayo, Guttmacher ilipata ongezeko la 7% la kiwango cha utoaji mimba kwa wanawake wenye umri wa miaka 15 hadi 44, kutoka 13.5 kwa kila wanawake 1,000 mwaka 2017 hadi 14.4 kwa kila wanawake 1,000.
Mjamzito mmoja kati ya watano aliishia kutoa mimba mwaka 2020, ongezeko la 12%, huku uwiano wa utoaji mimba ukiongezeka kutoka 18.4% mwaka 2017 hadi 20.6% mwaka 2020.
Kuanzia 2017 hadi 2020, ripoti hiyo ilibainisha kuwa  utoaji mimba uliongezeka kwa 12% Magharibi mwa Marekani na 10% katika eneo la kati magharibi, ambapo utoaji  mimba pia uliongezeka kwa 8% Kusini na 2% Kaskazini-mashariki.
Kwa mujibu wa utafiti wa  na Guttmacher ikinukuu data za mwezi februari mwaka huu kutoka Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia magonjwa inaeleza kuwa  ongezeko hili la utoaji mimba liliambatana na kupungua kwa asilimia 6 kwa watoto wanaozaliwa kati ya 2017 na 2020.
Siku ya Ijumaa,Mahakama ya juu zaidi nchini Marekani ilitoa uamuzi wake kwenye kesi ya utoaji mimba ambapo mahakama hiyo ilibatilisha haki ya wanawake kutoa mimba nchini Marekani.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.