MTANGAZAJI

WAMISIONARI WALIOTEKWA WAACHIWA HURU

 


 Wamisionari wa mwisho 12 ambao walikuwa wametekwa huko Haiti wameachiwa huru,Shirika la Kikristo linalojihusisha na Huduma ya Misaada (CAM) ambalo liliwapeleka nchini humo limeeleza.

Kundi la Wamisionari 17 walitekwa Oktoba mwaka huu likiwa njiani kutoka katika huduma ya kutembelea Kituo cha Watoto Yatima cha CAM huko Haiti.

Wamisionari hao 16 wanatoka Marekani na mmoja  Canada,ambapo pia lilijumuisha watoto na mdogo kuliko wote akiwa na miezi minane

Kikundi  400 Mawozo kilieleza kuhusika na utekaji huo ambapo lilitaka malipo ya fidia ya  Dola Milioni moja za Kimarekani kwa kila mtu ili kuwaachia.

Kiongozi wa watekaji hao  Wilson Joseph alitoa vitisho vya kuwaua wamisionari kama fidia  ama la wangewaua wamisionari.Wawili waliachiliwa Novemba huku watatu wakiachiliwa mwanzoni mwa mwezi huu.

CAM yenye makao yake makuu huko Ohio imethibitisha Disemba 16,2021 kuwa kundi lote la Wamisionari wameachiwa huru.


1 comment

Anonymous said...

LuckyClub Casino Site: The Lucky Club Casino Review
LuckyClub luckyclub.live Casino Review 2021. Sign up to get up to €100 + 20 FS today! Claim your welcome bonus now! Rating: 1.5 · ‎Review by LuckyClub.org

Mtazamo News . Powered by Blogger.