MTANGAZAJI

WAVUVI 12 WAPOTEZA MAISHA BWAWA LA MTERA.

  Wavuvi 12 wamepoteza maisha na wengine 15 kujeruhiwa katika kipindi cha mwezi wa pili 2020 hadi mwezi wa nane 2021 kufuatia matukio ya kuvamiwa na Viboko wakiwa ndani ya Bwawa hilo katika shughuli za uvuvi.
 
 Taarifa hiyo imetolewa ziara Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo ya kukagua Jitihada za Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori Tanzania TAWA za kukabiliana na wanyama waharibifu na wakali amewataka wavuvi kuzingatia njia sahihi za uvuvi salama ili kujilinda.
 
Moyo alibainisha kuwa miongoni mwa sababu za matukio hayo yalioondosha uhai ni pamoja na shughuli za Uvuvi kufanyika kwenye mazizi ya viboko,tabia ya wavuvi kutumia zana duni za uvuvi,kupungua kwa samaki katika Bwawa hilo na wavuvi kufanya shughuli ya uvuvi nyakati za usiku ambapo viboko wanakuwa katika harakati za kutoka nje kutafuta chakula.
 
Moyo aliyetembelea Bwawa la Mtera katika ziara ya kukagua jitihada za ziara yake ya kukagua Jitihada za Mamlaka ya Usimamizi Wanyamapori Tanzania TAWA za kukabiliana na wanyama waharibifu na wakali wakiwemo Viboko na Tembo ameeleza kusikitishwa na matukio hayo huku akitaja miongoni mwa sababu zinazochochea kuwapo kwa hatari dhidi ya wavuvi.
 
Moyo Amewaagiza maafisa Uvuvi, viongozi wa Serikali kwa ngazi zote kusimamia na  kuhamasisha  njia bora za uvuvi katika Bwawa la Mtera  ili kuepuka migongano ya Wanyama pori wakali na waharibifu akisisitiza kufuata miongozo na kanuni za uvuvi.
 

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.