MTANGAZAJI

WAADVENTISTA WA SABATO JIJINI MWANZA WANAVYOJIANDAA NA MKUTANO WA UFUNUO WA MATUMAINI


Kiongozi wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato Jimbo Kuu la Kaskazini mwa Tanzania akihutubia waumini wa Kanisa hilo kwenye uwanja wa CCM,Kirumba Mwanza


Kanisa la Waadventista Wa Sabato toka mitaa 13  ya jiji la Mwanza yenye makanisa mahalia 82 ambayo yanawaumini wapatao 33,308 walikusanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza April 14 mwaka huu katika Sabato maalum ya maandalizi ya mkutano wa Ufunuo wa Matumaini utakaoendeshwa na Mwinjilisti wa Kimataifa Mark Finley toka nchini Marekani Mei 12 hadi June 2 mwaka huu uwanjani hapo.

Siku hii maalum ambayo  pia ilihudhuriwa na kwaya zipatazo 54, viongozi wa  jimbo dogo  la Nyanza Kusini lenye mikoa ya Mwanza,Simiyu,Geita na Shinyanga hali kadhalika Viongozi wa Jimbo Kuu la Kusini mwa Tanzania na Jimbo Kuu la Kaskazini katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato wakiongozwa na Mwenyekiti wake Dr Gordwin Ole Lekundayo ambaye alitoa hotuba maalum ya ibada iliyosisitiza kuhusu umuhimu wa Habari Njema.
Alisema watu hupenda kusikia habari njema, mama kajifungua mtoto, mtoto amefaulu mitahani, nimepata mchumba, nimepanda cheo na mengine mengi husikia na kuyaona. Katika ulimwengu huu wenye kuhuzunisha Je, habari njema zinaweza kupatikana?,Hivyo mkutano wa Ufunuo wa Matumaini utaleta habari njema kwa jiji la Mwanza na Tanzania kwa ujumla.
-->

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.