MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:WAIMBAJI WA THE LIGHT BEARERS WAREJEA NCHINI TANZANIA TOKA UINGEREZA

 
 
 
 
 
Waimbaji 14 wa The Light Bearers ambao walisafiri kuelekea Reading,Nchini Uingereza kwa mkutano wa Injili ulioendeshwa na Mch Baraka Butoke toka Tanzania ambao ulikuwa umeandaliwa na Kanisa la Waadventista Wa Sabato Angaza la mjini humo ambako walikuwa huko kwa takribani majuma matatu.

The Light Bearers wamewasili saa saba mchana ya ijumaa ya Agosti 26,Mwaka huu katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa  Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam ambapo walipokelewa kwa kupewa zawadi ya maua na keki iliyoandaliwa na Kundi la Whatsapp la Marafiki wa Light Bearers ambalo imekuwa likishiriki kuratibu baadhi ya matukio ya waimbaji hao nchini na nje ya Tanzania.

Wakiwa nchini Uingereza waimbaji hao  wamefanikiwa kurekodi santuri mwonekano namba 3 na 4 ambazo nyimbo zake mbili mpya zimeshaanza kuoneshwa katika vituo vya televisheni na kwenye mitandao,pia walitembelea ofisi za Konferensi,Unioni na Divisheni zilizoko nchini humo.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.