MTANGAZAJI

MWANZA:MWENYEKITI WA BODABODA MKOANI MWANZA ATOA TAHADHARI JUU YA VITENDO VYA UKWAPUAJI

Mwenyekiti wa Chama cha Waendesha Pikipiki Mkoani Mwanza Makoye Kayanda (pichani), amewataharisha wakazi wa Jiji la Mwanza kuwa makini wawapo barabarani, ili kuepukana na vitendo vya ukwapuaji wa Mikoba na Mabegi vinavyofanywa na baadhi ya wahalifu kwa kutumia pikipiki.

Kayanda alitoa tahadhari hiyo jana Mwanza baada ya kupokea malalamiko ya kukithiri kwa vitendo vya ukwapuaji vinavyofanywa na baadhi ya watu wanaojifanya waendesha pikipiki, jambo linalochafua taswira ya waendesha pikipiki Mkoani Mwanza.

Tayari watu kadha wamefikisha malalamiko yao kwa uongozi wa bodaboda Mkoani Mwanza, baada ya kukumbwa na kadhia ya kukwapuliwa mikoba pamoja na mabegi yao, ambapo mmoja wa wahanga wa matukio hayo Diana Abdallah ameeleza kukwapuliwa mkoba wake uliokuwa na pesa pamoja na vito vya thamani wakati akitokwa kwenye shughuli zake.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.