MTANGAZAJI

SERIKALI KUSAMBAZA MADAKTARI BINGWA MAENEO YA PEMBEZONI IKIWEMO MKOA WA RUVUMA

dk kigwa9Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla akitoa ufafanuzi juu ya Wizara yake kuhakikisha itapeleka Madaktari bingwa katika mikoa mbalimbali nchini ikiwemo hospitali hiyo ya Mkoa wa Ruvuma wakati wa ziara yake aliyoifanya mapema Februari 13.2016.

Kauli hiyo ya serikali imetolewa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto mjini Songea, Dkt. Hamisi Kigwangalla baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Ruvuma na kituo cha afya cha Mjimwema kilichopo mjini Songea huku akiitaka mikoa ya pembezoni ukiwemo mkoa huo wa Ruvuma kuweka mazingira ya kuwavutia madaktari bingwa kufanya kazi katika mikoa yao.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bw. Said Mwambungu amesema kuwa mkoa huo umeridhishwa na staili ya ziara ya kushtukiza na kwamba wanajitahidi kuboresha vituo vya afya vya Mjimwema Songea, Madaba na cha wilaya ya Namtumbo ili vipandishwe hadhi kuwa hospitali za wilaya.

Pia Dk. Kigwangalla alipata wasaha wa kutembelea maeneo mbalimbali ya Hospitali hiyo na kujionea utendaji wa kazi huku akitoa wito katika suala la maboresho zaidi.

dk kigwa4

Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla (katikati) akijiandaa kuingia kukagua utendaji wa kazi na vifaa ndani ya chumba cha upasuaji cha Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma wakati wa ziara yake hiyo

dk kigwa

Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla akijiandaa kuingia kwenye chumba cha upasuaji wakati wa ziara yake hiyo, aliyoifanya mapema Februari 13.2016.

dk kigws

Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla akiangalia moja ya vitanda vinavyotumika katika upasuaji hospitalini hapo ambapo hata hivyo aliambiwa changamoto kuwa baadhi ya taa za vitanda hivyo kuwa na hitilafu wakati ziara hiyo hivi karibuni (Picha zote na Andrew Chale,modewjiblog-Songea, Ruvuma)

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.