MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:WASI WASI WA MVUA ZA EL-NINO NCHINI MWEZI SEPTEMBA MPAKA DESEMBA MWAKA HUU-TMA




 

Nchi za Afrika Mashariki na kati ikiwamo Tanzania zipo katika wasiwasi wa kukumbwa na mvua za El-nino kutokana na kuongezeka kwa joto katika Bahari ya Pacific.

Akizungumza kwenye mkutano wa 41 wa masuala ya hali ya hewa na utabiri unaofanyika jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA), Dk. Agness Kijazi (pichani)  amesema kitaalam kuna uwezekano wa kutokea kwa mvua kubwa katika nchi za Afrika Mashariki katika kipindi cha Septemba mpaka Desemba, mwaka huu.

Mkutano huo unawahusisha wataalam mbalimbali kutoka katika nchi 11 na unaangalia mifumo ya hali ya hewa kwa Afrika Mashariki na tayari wameona viashiria vya kutokea kwa mvua hizo.

Amesema baada ya kuangalia mifumo ya hali ya hewa katika eneo la Afrika Mashariki, wataalamu watarudi katika nchi zao na kuangalia mifumo ya hali ya hewa katika maeneo yao na kutoa utabiri kwa wananchi husika kwa kipindi cha mwez Septemba mpaka Desemba.  

 Kijazi ametoa wito kwa wananchi na wadau wa hali ya hewa kufuatilia utabiri utakaotolewa Septemba Mosi, mwaka huu ili kujua hali itakavyokuwa.




No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.