WHO KUSHIRIKIANA NA WAADVENTISTA WA SABATO KUPUNGUZA VIFO VYA AKINA MAMA NA WATOTO
Shirika la
Afya Duniani (WH0) na Kanisa la Waadventista Wa Sabato wameingia katika
ushirikiano wa mkakati wa
kiulimwengu katika kupunguza vifo vya
watoto na akina mama wakati wa kujifungua.
Annette
Mwansa Nkowane afisa toka WHO anaeleza kuwa hii ni mara ya kwanza kwa shirika
hilo linajihusisha na masuala ya afya
kuingia ubia na taasisi ya dini katika
mkakati wa miaka mitano kutoa mafunzo kwa wakunga.
Viongozi wa
wauguzi na wakufunzi 50 toka Amerika ya Kaskazini,Ulaya,Amerika ya Kusini na
Afrika juma hili wamekutana katika mji wa Bloemfontein, Afrika ya Kusini kwa
ajili ya kuzindua mradi huo ambao utaanza kutekelezwa katika nchi nne za
Afrika.
Mradi huo
ambao utagharimu dola milioni 1 za kimarekani umedhaminiwa na mradi wa
maendeleo wa kimataifa OPEC kupitia WHO na kuratibiwa na viongozi wa shirika
hilo na wale wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato duniani kupitia Chuo kikuu cha
utabibu cha Loma Linda.
Kwa mujibu
wa takwimu za WHO kiasi cha akina mama wajawazito 280,000 hufariki
wanapojifungua kila mwaka duniani huku ikielezwa kuwa Afrika ina asilimia 12 ya
madaktari na wakunga asilimia 30 ambapo idadi hiyo ni ndogo kutokana na
ongezeko la watu barani humo kwani hitaji ni kufundisha asilimia kumi hadi 30
ya madaktari.
Post a Comment