MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:JAMII YATAKIWA KUTOWADHALILISHA WENYE ULEMAVU



 
Mtoto akihubiri



Miriam Chirwa akiimba









Mtaalamu wa malezi ya watoto wa shule ya Uhuru mchanganyiko Mwalimu Betha Kayola ameitaka jamii kuacha kutumia majina ya kuwadhalilisha  watu wenye ulemavu.

Akizungumza mara baada ya ibada katika kanisa la Waadventista Wa Sabato Magomeni Mwembechai jana ambako kulikuwa na sabato maalum ya idara ya watoto, ambayo iliwaalika watoto wenye ulemavu kutoka shule ya uhuru mchanganyiko ya jijini Dar es salaam amesema kuwa, utumiaji wa majina yasiyofaa kwa watu wenye ulemavu ni kuwadhalilisha.

Mbali na maneno hayo ya udhalilishaji mtaalamu huyo amesema kuwa vitendo  vya udhalilishaji vimekuwa vikiendelea ndani ya jamii ambapo baadhi ya wazazi na walezi wamekuwa wakiwaficha watoto wenye ulemavu na hata kuwafanyia vitendo vya ukatili hivyo akaomba makanisa ya Waadventista Wa Sabato kuwa karibu na kituo hicho katika kuwasaidia watoto wa shule ya uhuru Mchanganyiko.

Jumla ya watoto 55 na walezi watatu  toka Shule ya Uhuru Mchanganyiko walihudhuria katika sabato hiyo ya wageni  ambayo iliongozwa na watoto wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato Magomeni Mwembechai ambapo Mtoto mwenye ulemavu Miriam Chirwa aliimba.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.