MTANGAZAJI

PWANI:HOSPITALI YA WILAYA YA MKURANGA HAINA X-RAY



Wakazi wa wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani  wameilalamikia hospitali ya wilaya hiyo kwa kutokuwa na  huduma ya x-ray na hivyo kuwalazimu wakazi hao kwenda  kupata huduma hiyo katika hospitali za taifa Muhimbili jijini Dar es salaam.

Wakazi hao wamesema kuwa kukosekana kwa huduma ya X-ray katika hospitali hiyo kuna wasababishia  gharama za kwenda muhimbili jijini Da es salaam kwa ajili ya kupata huduma.

Mwenyekiti wa chama cha  maendeleo  chadema wilayani humo Rwey Jamal amesema kuwa hospitali hiyo haikutakiwa kuitwa hospitali badala yake ingeitwa kituo cha afya kwani kutokuwepo kwa huduma hiyo ni tatizo kubwa hasa kwa hospitali ya wilaya.

Mganga mkuu wa hospitali hiyo Dr Francis Manisi amethibitisha kutokuwepo kwa mashine hiyo   na kudai kuwa wako mbioni kuweka huduma hiyo kwani imekuwa changamoto kubwa kwa wagonjwa hali ambayo huwafanya walipe kiasi kikubwa cha fedha kwenda katika hospitali ya taifa

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.