MTANGAZAJI

MARA:MWANAMKE AUAWA KUTOKANA NA WIVU WA MAPENZI



Mwanamke aliyetambulika kwa jina la Mariam Matiko (20) mkazi wa Kitongoji cha Romboni kijiji cha Nyangoto katika mji wa Nyamongo wilayani Tarime amekutwa amefariki dunia ndani ya nyumba yake akiwa ametapakaa damu mwili mzima bila kuwa na jeraha lolote.

Tukio  hilo lilitokea julai 18 mnamo saa 7.30 wakati majirani walipogundua kuwa dada huyo alikuwa haonekani kwa masaa kadhaa kisha kutoa taarifa kituo cha polisi cha Nyangoto ambao walifika eneo hilo kwa ukaguzi na kumkuta mwanamke huyo akiwa amefariki huku amefungwa khanga shingoni.Mumewe mariamu alitajwa kuwa ni Mwita Mtumba anayedaiwa kuwa alimuua mkewe kutokana na wivu wa mapenzi kwa kumhisi kuwa na mahusiano na mwanamume mwingine na hili ni tukio la pili katika eneo la Nyamongo baada ya lile la mwanamke kuchomwa sehemu zake siri na mwanaume.

Kwa mjibu wa taarifa ya Mganga Mfawidhi wa kituo cha afya Nyamongo Kagumilwa Kaijage kwa ushirikiano na jeshi la polisi, ukaguzi uliofanywa unaonesha marehemu alikuwa mekaa kwenye kiti akiwa amefungwa khanga shingoni, lakini haikuonekana kuwa ana alama yoyote ya kujinyonga na ndipo  mwili ulipelekwa chumba cha kuhifadhia maiti kilichoko kituo cha afya Nyamongo lakini ndugu wa marehemu walimchukuwa na kwenda kumzika baada ya kuelewana na upande wa mwanamume watalipa ng’ombe watano.

 Kamanda wa polisi kanda maalumu ya Tarime Rorya kamishina msaidizi Lazaro Mambosasa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa mtuhumiwa baada ya kutenda kosa hilo alitorokea kusiko julikana na jeshi la polishi linafanya juhudi za kumtia mbaroni.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.