MTANGAZAJI

RORYA:WAUMINI WA DINI MBALIMBALI WATAKIWA KUWA NA USHIRIKIANO



Waumini wa dini mbalimbali wametakiwa kuwa na ushirikiano katika shughuli za kiroho ili kukuza mahusiano mazuri na kujenga umoja bila kubaguana kwa sababu za kiitikadi.

Kauili hiyo ilitolewa na mwenye kiti wa kijiji cha Deti Sebastiani Okaro wakati wa harambee ya kuchangia vyombo vya muziki vya kanisa la Waadventista Wasbato la Radienya lililoko kata ya Labuor Wiyani Rorya.

Okaro ameyasema hayo baada ya kuona kuwa hakuna waumini wa dhehebu liingine walioalikwa kutoa michango yao hali ambayo iliwafanya waumini hao kushindwa kufikia malengo waliyojiwekea.

Amesema kuwa endapo madhehebu yatakuwa na umojo wa kiundungu wataongeza imani kwa wale ambao hawajaamua kumfuata Mungu na kwanjia hiyo tabia na mienendo yao itabadilika na kupunguza uharibifu katika Wilaya hiyo.

Naye mgeni rasmi wa harambee hiyo Cuthbert Simion aliwataka waumini kutumia mali zao katika ujenzi wa makanisa kama ilivyo wanavyotoa kwenye harusi na  misiba.

Katika harambee hiyo zaidi ya sh.2.1 milion zilikusanywa kwa ajili ya ununuzi wa vyombo vya muziki vitakavyo wafanya waimbaji wa kwaya ya kanisa hilo kumtukuza Mungu ndani na nje ya Wilaya ya Rorya huku lengo likiwa ni kupata sh, 3.5 milioni.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.