MTANGAZAJI

ARUSHA:WAKAZI WA TEMI YA SIMBA WAOMBA MSAADA




Wakazi wa  kijiji cha Temi ya simba kata ya bwawani akipokea misaada 

 

Wananchi wa kitongoji cha Nyamagana,kijiji cha Temi ya Simba,kata ya Bwawani katika Jimbo la Arumeru Magharibi mkoani Arusha wameziomba Taasisi mbalimbali za kiserikali na Dini kuongeza misaada zaidi ya chakula,malazi,na mavazi kutokana na maafa ya mafuriko yaliyowapata kati ya mwezi wa April na Mei mwaka huu.



Akizungumza na Vyombo vya Habari hivi karibuni kwa niaba ya wananchi mwenyekiti wa kijiji cha Temi ya Simba Emanuel wiliam Molel  amesema kuwa wanakijiji hao wanakabiliwa na njaa,Malazi,mavazi pamoja na Nyumba baada ya mafuriko kutokea mnamo machi 23 Mwaka 2014 na kuathiri shughuli za kiuchumi katika eneo hilo.



Kwa mujibu wa Taarifa kutoka kwa mwenyekiti huyo  Nyumba Arobaini na Tisa zilianguka hivyo kuwafanya wakazi wa kijiji hicho kukosa makazi.



Kanisa la waadventista wasabato Kijenge limekabidhi kwa wananchi hao misaada yenye  thamani ya shilingi milioni moja za kitanzania,misaada hiyo ni mahindi,maharage,na Nguo.Hata hivyo serikali ya kijiji iliweza kuwapatia pia Magodoro,Nguo na chakula.










No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.