MTANGAZAJI

WAKALA WA MAABARA YA MKEMIA MKUU WA SERIKALI YAANDAA SEMINA YA MATUMIZI SALAMA YA KEMIKALI KWA WAANDISHI WA HABARI NA TAASISI MBALIMBALI

Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali na Msajili wa Kemikali za Viwandani na Majumbani ameandaa mafunzo juu ya Matumizi Salama ya Kemikali kwa ajili ya waandishi wa vyombo vya habari (TV,Radio na Magazeti) na asasi zisizo za kiserikali zinazojihusisha na utoaji wa elimu kwa umma kuhusu matumizi salama ya Kemikali.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa ufunguzi wa mafunzo. Mafunzo hayo yanafanyikia kwenye ukumbi wa Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali uliopo ndani ya jengo la "Mkemia House" barabara ya BarackObama (Zamani Ocean Road)
 Washiriki wa mafunzo wakifuatilia Mafunzo
Kaimu Mkemia Mkuu wa Serikali Ndugu Samanitho Mtega (Katikati) akifungua mafunzo juu ya Matumizi Salama ya Kemikali. Kushoto kwake ni Bi. Everlight Matinga-Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi na Udhibiti wa Kemikali. Kulia kwa Kaimu Mkemia Mkuu wa serikali ni Kaimu Meneja wa Kanda ya Mashariki ndugu Daniel.

Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi ya Makosa ya Jinai (Forensic Science) na Vinasaba  Bi. Gloria Cuthbert Omary ametoa wito kwa waandishi wa Habari kuwa kiungo kati ya Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali na Jamii katika kuelimisha na kuleta upatanisho kati ya taasisi hiyo na Jamii ili jamii iweze kujifunza na kuelewa juu ya kazi mbalimbali zinazofanywa na Wakala hiyo.



Bi. Gloria amesema kuwa waandishi wa habari wana wajibu wa pekee katika kujenga taifa kwa kuandika habari zilizo sahihi kutoka mamlaka husika na kuongeza kuwa kwa kufanya hivyo watatoa mwanya kwa wanajamii na wadau mbalimbali kuchangia kwa usahihi hoja na mijadala inayohusiana na kazi au matokeo ya Uchuguzi unaofanywa na Wakala wa Mabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali nchini Tanzania.

 WADAU WA KEMIKALI WAZINGATIE SHERIA NA KANUNI

Wadau wa Kemikali nchini wametakiwa kufuata Sheria na Kanuni wakati wa kuingiza, kusafirisha, kuhifadhi, kuuza, kusambaza na wakati wa kutumia kemikali hizo ili kuepusha madhara yanayoweza kuletwa na matumizi yasiyo salama ya kemikali.



Hayo yamesemwa na Bi. Everlight Matinga ambaye ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi na Udhibiti wa Kemikali (katika ofisi ya Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali) wakati akitoa ufafanuzi kwenye mafunzo hayo kuhusu sheria ya Kemikali za Viwandani na Majumbani ambayo lengo lake ni kulinda afya za wananchi na mazingira

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.