MTANGAZAJI

TAKWIMU ZA HUDUMA ZA KIJAMII NCHINI TANZANIA



Utafiti wa Viashiria vya VVU,UKIMWI na Malaria Tanzania kwa mwaka 2011 hadi 2012 uliofanywa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa kushirikiana na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Zanzibar unaonesha kuwa,Kaya nchini Tanzania zinawastani wa watu watano,karibu robo ya kaya zinaongozwa na wanawake,Karibu nusu ya wananchi wana umri chini ya miaka 15.

Hali ya maisha imekuwa bora kwa kiasi Fulani katika maeneo ya mijini Tanzania bara na Zanzibar kuliko maeneo ya vijijini Tanzania Bara.
Karibu kaya tisa kila kaya kumi za mijini Tanzania Bara zinapata maji ya kunywa kutoka katika chanzo kilichoboreshwa,ukilinganisha na  asilimia 47 ya kaya za vijijini Tanzania Bara.

Karibu kila mahali Zanzibar kuna vyanzo vya maji ya kunywa vilivyoboreshwa.Huduma za usafi wa mazingira zipo kiwango kidogo nchi nzima asilimia 26 kwa kaya za mjini Bara na asilimia 7 tu ya kaya za vijijini Bara ndizo zenye huduma bora za usafi wa mazingira.
Kaya sita katika kila kaya kumi Zanzibar zinapata huduma bora ya usafi wa mazingira.

Asilimia 15 ya kaya Tanzania ndizo zenye umeme,idadi imeongezeka kidogo kutoka asilimia 12 ya mwaka 2007 na 2008.Tanzania Bara kuna tofauti kubwa katika upatikanaji wa umeme baina ya kaya za mijini na vijijini  ambapo ni asilimia 46 tu. Kwa upande wa Zanzibar asilimia 41 ya kaya ndio zenye umeme.

Zaidi ya asilimia 60 ya kaya nchini Tanzania zina redio,wakati asilimia 15 tu ndizo zenye tv,Asilimia sitini na moja ya kaya zina simu ya mkononi.Karibu kaya moja katika kila kaya tano zina akaunti  benki.Karibu nusu ya kaya zina baiskeli wakati asilimia 2 tu ya kaya zina gari dogo au lori.

Asilimia kumi na nane ya wanawake wenye umri wa miaka 15-49 na asilimia 9 ya wanaume wenye umri huo hawana elimu.Zaidi ya nusu ya wanawake na wanaume wamehitimu elimu ya msingi.Ambapo asilimia moja tu ya wanawake na asilimia 2 ya wanaume wamehitimu elimu ya sekondari ama zaidi.

Wanaume wanauwezekano mkubwa wa kupata habari kupitia vyombo vya habari kuliko wanawake nchini Tanzania.Zaidi ya asilimia 40 ya wanawake hawakuwa na uwezo wa kupata taarifa kupitia vyombo vya habari angalau kwa kila juma ukilinganisha na asilimia 23 tu ya wanaume.

Redio ni njia inayotumiwa na wengi kupata taarifa kwani asilimia 74 ya wanaume na asilimia 49 ya wanawake wanasikiliza redio kila juma.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.