MTANGAZAJI

TAKWIMU ZA AJALI ZA BARABARANI KWA MWAKA 2012 NCHINI TANZANIA



 


Takwimu  za Jeshi la Polisi Tanzania kitengo cha Usalama Barabarani kuhusu hali ya ajali za barabarani kwa mwaka 2012 zilizopo kwenye ripoti ya haki za binadamu iliyozinduliwa mwaka huu zinaonesha kuwa mwaka 2012 kulikuwa na ajali 11438 na ambazo lilisababisha vifo vya watu 4919.

Katika takwimu hizo zinaonesha kuwa   Mbeya kulikuwa na ajali 617 waliokufa ni 309,Pwani ajali 1330 waliopoteza maisha ni 238,Kilimanjaro ajali 1502 na kuua watu 208,Morogoro watu 285 walipoteza maisha yao kutokana ajali 1599,Ambapo mkoani Arusha kulikuwa na ajali 2136 ambazo zilisababisha vifo vya watu 192 na Iringa kulitokea ajali 791 zilizopoteza maisha ya watu 195,Mwanza ajali 533 na kuua watu 235,Dar es salaam ndio inaonekana kuongoza kwa kuwa na ajali 2930 zilizosababisha vifo vya watu 431.

Kwa upande wa ajali zilizosababishwa na pikipiki ama bodaboda takwimu zinaonesha zilisababisha vifo vya watu 695 kwa mwaka 2011 na mwaka 2012 watu 930 ambayo ni tofauti ya watu 235 ambapo mwaka 2010 kulikuwa na vifo vya watu  647 zilizosababishwa na pikipiki ikiwa ni tofauti ya watu 48 kwa mwaka 2010 na 2011.

Miongoni mwa sababu za ajali hizo ni uzembe wa madreva na kutofuatwa kwa sheria za usalama barabarani

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.