MTANGAZAJI

TAMKO LA NEC JUU YA KUPANDA KWA GHARAMA ZA MAISHA NCHINI.


Halmashauri Kuu ya CCM Taifa imejadili kwa kina suala la kupanda kwa
gharama za maisha nchini. NEC inakiri kwamba ni kweli lipo tatizo la
kupanda kwa gharama za maisha nchini. Tatizo hili pia limezikumba
karibu nchi nyingi za Afrika Mashariki na kwakweli karibu sasa lipo
dunia nzima. Baadhi ya sababu za kupanda kwa gharama za maisha hapa
nchini ni pamoja na;

1. Hali mbaya ya mavuno inayotokana na uhaba wa mvua au mvua kunyesha

     kipindi cha nje ya msimu katika maeneo mengi nchini.
2. Kuongezeka kwa bei ya mafuta duniani, hivyo kuongezeka kwa gharama
     za uzalishaji wa bidhaa na usafirishaji wa mazao.
3. Kuyumba kwa thamani ya dola ya Marekani.
4. Kuwepo kwa soko huria ambapo sasa mazao ya chakula yanapata soko
    nje ya nchi, na wakati mwingine kuuzwa nje kwa njia ya magendo na
    hivyo kusababisha uwepo wa ukubwa wa mahitaji na hivyo kuongezeka kwa
    bei ya chakula nchini.
5. kuongezeka kwa walaji wakati uzalishaji ukiwa mdogo.
6. kutofanikiwa (ikiwemo kuhujumiwa na wafanyabiashara wasio
waaminifu) kwa baadhi ya mikakati ya kudhibiti mfumko wa bei.
Uwamuzi wa Halmashauri Kuu ya Taifa.

1. Pamoja na Serikali kuendelea kuchukua hatua za muda mrefu na wa

   kati za kukabiliana na tatizo hili, CCM inaiagiza Serikali kuchukua
   hatua za haraka za muda mfupi ikiwemo kuangalia upya baadhi ya kodi
   katika vyakula pamoja na kodi ya ongezeko la thamani VAT katika
   sukari.

2. Utaratibu wa ruzuku ya mbegu na mbolea upanuliwe ili kunufaisha

     wakulima wengi.
3. Serikali iongeze kasi ya utekelezaji wa mpango wake wa kuongeza
    uwezo wa kuhifadhi chakula nchini, hasa kwa kupitia Hifadhi ya Nafaka
   ya Taifa, ikiwa ni pamoja na kujenga maghala zaidi ya mazao ya chakula
   katika maeneo ya uzalishaji wa mazao, na kutenga fedha nyingi zaidi
   kwa ununuzi wa mazao hayo. Pamoja na hili, mipango ifanywe kuongeza
   uwezo wa wakulima kuhifadhi chakula chao wenyewe na kupunguza upotevu
  baada ya mavuno (post-harvest losses).
3. Serikali iendelee kupanua utaratibu wake wa kutumia Hifadhi ya
    Nafaka ya Taifa (SGR) kama nyenzo ya kudhibiti kupanda kwa bei za
    vyakula. Wakati wa uhaba wa vyakula katika maeneo ya mijini, kasi ya
   kupeleka chakula maeneo hayo iongezwe na utaratibu mzuri zaidi wa
   usambazaji wa chakula utumike ili walaji, na sio wasafirishaji na
   wasindikaji, wanufaike.

4. Serikali iongeze kasi ya utekelezaji wa miradi mikubwa ya kilimo

    nchini, hasa ASDP na SAGCOT, ambayo itasaidia kumaliza tatizo la
    chakula nchini na kuongeza ajira na kipato kwa Watanzania walio
    wengi.
5. Serikali idhibiti malipo ya huduma ya ndani kwa kutumia fedha za
    kigeni, hasa dola za kimarekani. Aidha, Serikali iongeze udhibiti wa
   Maduka na mahoteli yanayofanya biashara ya fedha za kigeni ili kuondoa
   hujuma kwa uchumi wa nchi inayofanywa kutokana na uhuru uliokithiri
   katika biashara hii.
6. Waajiri wahimizwe kupandisha mishahara na malipo mengineyo kwa
     wafanyakazi wao ili waweze kumudu gharama za maisha.
7. Serikali iweke jitihada zaidi za kudhibiti ulanguzi wa bidhaa
    muhimu na upandishaji holela wa bei za vyakula, kodi za nyumba na
   usafiri.

Nape Moses Nnauye Chama Cha Mapinduzi
Ideology and Publicity Secretary

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.