MTANGAZAJI

JE WAJUA VUVUZELA LINA MADHARA???

VUVUZELA chombo kilichotumika kwa kushangilia hasa na mashabiki wa soka kwenye Kombe la Dunia la soka mwaka 2010, si tu kinachafua mazingira kwa kelele, wataalamu wanadai chombo hicho kinaweza kusababisha maradhi kiafya mpulizaji.

Inaeleza kwamba upulizaji kidogo tu wa Vuvuzela mfanya mpulizaji atokwe na mate mengi sawa na yanayotoka wakati mtu akipiga chafya, tena yenye uwezo wa kusafiri hewani kwa mwendo kasi mara milioni nne kwa sekunde moja kwa kila tone, hii ni kwa mujibu wa jarida moja la kimataifa

Inaelezwa kuwa eneo lililofurika watu, mtu mmoja akipuliza vuvuzela linaweza kuwaathiri watu wengi kwa magonjwa yanayosambazwa kwa kuvuta hewa kama mafua na kifua kikuu.

Hata hivyo, Dk. Ruth McNerney, aliyeendesha utafiti wa hivi karibuni katika shule inayohusika na masuala ya usafi na maradhi ya nchi za joto ya London – London School of Hygiene & Tropical Medicine, anasema “upulizaji wa chombo cha vuvuzela” huenda kinahitajika kuliko kukipiga marufuku.

“Kama ilivyo wakati wa kukohoa na kupiga chafya, hatua zinapaswa kuchukuliwa kuzuia uenezaji wa maradhi, na watu wenye maradhi ya kuambukiza washauriwe wasipulize vuvuzela zao karibu na watu”, alisema.

Kamati yake iliyochunguza hatari zinazoletwa na upulizaji wa vuvuzela, waliowatumia watu wanane waliojitolea kupuliza vuvuzela. Kwa wastani chembechembe zinazotoka kwenye mapafu, 658,000 kwa lita ya hewa zilitolewa kutoka kwenye vuvuzela.

Matone hayo ya mate yaliruka angani kwa kiwango cha mara milioni nne kwa sekunde. Kwa kulinganisha, wakati watu hao waliojitolea walipotakiwa kupiga kelele, waliweza kutoa mate kiasi cha chembechembe 3,700 tu kwa lita kwa kiwango cha 7,000 kwa sekunde.

Toka:BBC Swahili

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.