MTANGAZAJI

MKUTANO MKUU WA KANISA LA WAADVENTISTA ULIMWENGU (GC) KUTOFANYIKA MWAKA HUU



 Kamati ya Utendaji ya Kanisa la Waadventista wa Sabato Ulimwenguni iliyoketi Machi 19 mwaka huu  imeaihirisha Mkutano Mkuu wa Kanisa la Waadventista Ulimwenguni  uliokuwa ufanyike Indiana nchini Marekani mwaka 2020 hadi Mei 2021.

Tovuti ya Makao Makuu ya Kanisa hilo imeeleza kuwa Kikao cha Kamati hiyo  kilichofanyika kwa njia ya teknolojia ya masafa inayowezeshwa na intaneti kimewahusisha  wajumbe wake walioko katika nchi mbalimbali Duniani.

Uamuzi huo umepigiwa kura na kupitishwa na kikao hicho baada ya mapendekezo ya Machi 17,2020 yalitolewa na Kikao cha Kamati ya Uongozi ya Kanisa hilo (ADCOM) kuahirisha Mkutano huo kwa muda wa miaka miwili kutokana na janga la  ugonjwa wa Covid-19  lilozikumba nchi mbalimbali duniani.

Kikao hicho kimepitisha kuwa ni wajumbe tu  ambao watahudhuria Mkutano Mkuu wa mwakani , hakutakuwa na mabanda ya taasis mbalimbali  kama ilivyokuwa ikifanyika awali na kipindi cha Uongozi wa Kanisa hilo kitaendelea kama kawaida.
 
Mkutano Mkuu wa Kanisa hilo Ulimwenguni kwa mwaka 2021 umepangwa kufanyika Indianapolis, Indiana nchini Marekani  Mei  20 hadi  Mei 25,Awali ilikuwa ufanyike It was originally scheduled Juni 25 hadi  July 4, 2020. 

Janga la Ugonjwa wa Covid-19 limesambaa duniani toka mwaka 2019,Januari 30,Shirika la Afya Duniani (WHO) lilitangaza kuwa ugonjwa huo ni janga la Dunia,ambapo mpaka sasa virusi vya ugonjwa huo vimeathiri zaidi ya watu 230,000 huku zaidi  ya  vifo vya watu  9,300 wakitokana na ugonjwa huo.

Kanisa la Waadventista wa Sabato Ulimwenguni lenye makao yake Makuu

1 comment

Unknown said...

Amen. God Cares! Let's play our part.

Mtazamo News . Powered by Blogger.