MTANGAZAJI

WAZAZI WATAKIWA KUTOWATENGA WATOTO WENYE ULEMAVU

 Mbunge wa viti maalumu CCM Amina Mollel akiwa anacheza ngoma ya kimasai pamoja na baadhi ya wamasai waliojitokeza katika sherehe za   kupandisha ngazi ya  rika kutoka katika rika la kurianga kuingia katika rika la Nyangulo (Habari picha  na  woindeshizza blog )

Mbunge wa viti maalumu CCM Amina Mollel akiwa anasalimia na moja na mzee aliyekuwa rika la kurianga ambae kwa sasa ameingia katika rika  la Nyangulo   


Wazazi hususani wa jamii ya kimasai wametakiwa kuachana na dhana ya kuwatenga na kutowapeleka shule watoto wa kike na wale ambao ni walemavu  badala yake wawapeleke mashuleni kwani wao ndio viongozi wa baadae

Hayo yamebainishwa na mbunge wa viti maalumu  (CCM) Amina Mollel wakati alipokuwa akizungumza  katika sherehe za  kupandisha ngazi rika kutoka katika rika la kurianga kuingia katika rika la Nyangulo ,sherehe ambazo zilifanyika katika   Kijiji cha Oldenderet Kata ya Nduruma mkoani Arusha

Alisema kuwa kunabaadhi ya wazazi wamekuwa wakiwaficha  watoto wao kisa ni walemavu jambo ambalo linawakosesha haki zao ikiwemo ya kupata elimu  kutokana na kufichwa huko.
Pia amewataka wazazi wa jamii ya kimasai na hata wale wa makabila mengine kuacha kuwaozesha watoto wakike mapema kwani watoto hao wakike nao wanahaki ya kupata elimu kwani elimu ni bure ,kuanzia  ngazi ya msingi hadi sekondari hivyo ni vyema kama wazazi wakawasimamia watoto hususa ni wakike wakaenda shule

Alisema kuwa kunabaadhi ya watoto wa kike wamekuwa wanaacha kusoma kisa wanakimbilia maisha kitu ambacho sio kizuri kwani wanaweza kukimbilia maisha yakawapiga hivyo ni muhimu sana kama watasoma kwanza alafu maisha watayapata baadae baada ya kumaliza kusoma na kupata kazi zao nzuri

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.