MTANGAZAJI

WAKULIMA WILAYA YA CHATO WAFURAHIA KUPATA MBEGU BORA KUTOKA COSTECH

 Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi na Viumbe Hai wa COSTECH, Dk.Bakari Msangi (kushoto), kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), akimkabidhi mbegu ya viazi lishe kwa ajili ya shamba darasa la Kijiji cha Kibehe, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato, Mhandisi Joel Hari wakati wa uzinduzi wa shamba hilo wilayani Chato leo. 
 Wanakikundi cha Umoja cha Kijiji cha Kibehe kilichopo Kata ya Kigongo wakiandaa shamba lao la mbegu.
 Wanakikundi cha Umoja cha Kijiji cha Kibehe kilichopo Kata ya Kigongo wakiwa kwenye uzinduzi wa shamba darasa la viazi lishe na mihogo.
 Mtafiti wa Mazao ya Mizizi wa Wilaya ya Chato, Monica Mulongo akizungumzia vitamini A inayopatikana kwenye viazi lishe ambayo ni muhimu kwa watoto.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi na Viumbe Hai wa COSTECH, Dk.Bakari Msangi, akizungumza wakati wa uzinduzi wa shamba darasa la mbegu ya viazi lishe. Kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato, Mhandisi Joel Hari.
 Mtafiti Ismail Ngolinda kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Ilonga mkoani Morogoro akizungumzia ubora wa mbegu ya Wema pamoja na upandaji wake.


 
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya ya Chato, Mhandisi Joel Hari , akionesha mbegu ya mahindi ya Wema baada ya kukabidhiwa.

 Mtafiti wa mazao ya mizizi kutoka Kituo cha Utafiti cha Maruku mkoani Kagera, Jojianas Kibula, akiwaonesha wakulima wa Kibehe jinsi ya kupanda mbegu ya mhogo.


 Mshauri wa Jukwaa la ioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo (OFAB), Dk.Nicholaus Nyange akipanda mbegu ya mhogo katika shamba darasa la Kijiji cha Itale.
 Wakulima wa Kijiji cha Bukiliguru wakishiriki kuapanda mbegu za mahindi katika shamba darasa.


Wakulima wa Wilaya Chato mkoani Geita wamefurahia mbegu bora ya mihogo, mahindi na viazi lishe waliopewa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) ili kuanzisha mashamba darasa ya mbegu hizo na kuzisambaza kwa wakulima wengine katika maeneo mengine.

Wakizungumza wilayani hapo kwa nyakati tofauti wakati wa uzinduzi wa mashamba darasa ya mbegu hizo katika vijiji vya Kibehe, Ipandikilo, Kitongoji cha Kaseni, Kijiji cha Itale na Bukiliguru kilichopo Kata ya Bwanga walisema mbegu hizo walizokabidhiwa na COSTECH kwa kushirikiana na Jukwaa la Bioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo ni mkombozi kwao.

Ofisa Kilimo wa Kata ya Kachwamba,  Hamisi  Matesi alisema Costech kuwapelekea wakulima mbegu hizo itawasaidia sana kupata chakula wananchi wa kata hiyo ziada watauza.

Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Ipandikilo, Clara Fidelis akizungumza kwa niaba ya wananchi wa kijiji hicho alisema wakulima walikuwa wakipata mavuno machache ya mahindi na mihogo kwa kuwa hawakuwa na mbegu bora hivyo baada ya kufunguliwa kwa shamba darasa la mbegu hizo katika maeneo yao wanategemea kupata mazao mengi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya ya Chato, Mhandisi Joel Hari aliwataka wananchi hao kutambua kuwa mpango huo wa serikali ya awamu ya tano unawategemea sana wakulima katika kilimo hivyo fursa hiyo walioipata ya kupelekewa mbegu hizo wasiipoteze.

Hari ameishukuru COSTECH kwa kuamua kuipatia wilaya hiyo mashamba darasa katika vijiji hivyo kwani anaamini mbegu hizo zitasimamiwa vizuri na kisha kuwafikia wakulima wengi zaidi ili waweze kuachana na mbegu zao za zamani ambazo zinashambuliwa na magonjwa ya batobato na michirizi ya kahawia.

Akizungumza kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH wakati wa kukabidhi mbegu hizo, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi na Viumbe Hai wa COSTECH, Dk.Bakari Msangi alisema kazi kubwa ya COSTECH ni kuishauri serikali katika masuala yote yanayohusu  Sayansi na Teknolojia na kusimamia tafiti zote za kisayansi katika maeneo mbalimbali na kilimo na kuhakikisha matunda ya tafiti hizo yanawafikia walengwa.

Alieleza kuwa mbegu hizo walizozikabidhi ikiwamo ya mahindi yanayostahimili ukame ya Wema 2109 zimefanyiwa utafiti na zitapandwa katika mashamba darasa na baadae kusambazwa kwa wakulima wengine ili kuondoa changamoto ya kukosekana kwa mbegu bora kutokana na wakulima kukabiliwa na mbegu ambazo zilikuwa na magonjwa kama batobato katika mihogo.
Na Dotto Mwaibale





No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.