MTANGAZAJI

KIONGOZI WA KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO DUNIANI YUKO NCHINI RWANDA


 

Kiongozi  wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato Duniani Mch Ted  Wilson ameweka jiwe la Msingi la Chuo Kipya  cha Udaktari cha Waadventista nchini Rwanda

Wilson ambaye ni mara yake ya pili kufika nchini humo toka awe Kiongozi wa Kanisa hilo baada ya kufanya hivyo mwaka jana aliweka jiwe hilo la msingi kwenye jengo la Chuo hicho ambalo litagharimu dola za kimarekani milioni 6.1 liko Masoro kwenye Chuo Kikuu cha Waadventista Wa Sabato cha Afrika Mashariki na Kati  cha Kigali,Rwanda .

Sehemu ya kwanza ya ujenzi wa chuo hicho itahusisha sehemu ya wanafunzi wa kike na wa kiume,eneo la kulia chakula,mahali  pa kulala wageni,na litafunguliwa kwa ajili ya wanafunzi Septemba 2017.

Kiongozi huyo ambaye ameambatana na mkewe Nancy amepata nafasi ya kufanya mazungumzo na Rais wa Rwanda Paul Kagame  atakuwa nchini humo ikiwa ni sehemu ya ushiriki wake katika mikutano ya injili ya majuma mawili iliyoanza ijumaa  jioni ambapo watu 100,000 wanatarajiwa kubatizwa ifikapo Mei 28 mwaka huu.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.