MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:TAARIFA YA KONGAMANO LA KIMATAIFA LA UTAFITI WA MAGONJWA YA BINADAMU HII HAPA


 

Kongamano la  Wanasayansi  lililoandaliwa na Taasisi  ya Magojwa ya Binadamu nchini Tanzania  linatarajiwa kufanyika  Oktoba 29 mwaka huu katika ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es salaam.


Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Magojwa ya Binadamu Tanzania  Dr Mwele Malecela (Pichani)  amesema  lengo  la Kongamano  hilo ni kuwakutanisha watafiti,watunga Sera,watoa maamuzi,wananchi  na wadau wengine wa tafiti za afya  kutoka ndani na nje ya Tanzania ili kuwakisisha na kujadili  matokeo ya Tafiti mbalimbali za uimarishaji wa afya na hali bora ya Maisha.


Malecela amesema kongamano hilo litaambatana na  Maadhimisho  ya miaka 35 ya taasisi ya taifa  ya utafiti wa magojwa ya binadamu na Kumbukumbu za miaka 120 za utafiti wa Afya Tanzania na mada zitakazozungumziwa zitalenga Tafiti za magojwa,mifumo ya huduma za Afya na  Visababishi vya Maradhi  katika Jamii.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.