MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM: MKE WA RAIS WA TANZANIA MAMA SALMA KIKWETE AWATAKA WANASIASA KUTOENEZA SIASA ZA CHUKI NCHINI HUMO

Mama Salma Kikwete akiwa na Kiongozi wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato Unioni ya Kusini mwa Tanzania Mch Mark Walwa Malekana

Mama Salma Kikwete akiwapungia mkono wananchi waliohudhuria tamasha la kuombea amani Tanzania



Mama Salma Kikwete akihutubia


 
Mchungaji Mark Walwa Malekana ambaye ni Kiongozi wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato Tanzaia  akisoma maelezo ya tuzo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete  kabla ya kuikabidhi kwa Mama Salma Kikwete
Mama Salma Kikwete akipokea tuzo ya Rais Jakaya Kikwete toka kwa Mch Mark Walwa Malekana iliyotolewa na Kampuni ya Msama Promotion



Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda akihutubia kwenye Tamasha la Kuombea Amani Tanzania lililofanyika Uwanja wa Taifa Oktoba 4,2015


Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Salma Kikwete amewataka wanasiasa na wafuasi wao kutoeneza siasa za chuki ambazo zinaweza kuwatenga wananchi kwa misingi ya dini,ukabila,ukanda kwa kuwa jambo hilo ni hatari kwa taifa la Tanzania  pia kutofanya kampeni katika nyumba za ibada.

Mama Salma Kikwete alitoa agizo hilo wakati akihutubia maelfu ya waumini wa madhehebu ya mbalimbali ya dini nchini Tanzania katika Tamasha la Kuombea Amani kabla ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 25 mwaka huu  lililofanyika kwenye uwanja wa michezo wa Taifa jijini Dar es salaam Oktoba 4,2015  ambapo pia lililowahusisha viongozi wa madhehebu hayo na waimbaji wa nyimbo za injili toka Tanzania,Kenya,Zambia,Afrika Kusini na Uingereza.

Naye Kiongozi wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato Unioni ya Kusini mwa Tanzania Mchungaji Mark Walwa Malekana akikabidhi tuko ya Rais Jakaya Kikwete kwa Mama Kikwete amesema amani ya Tanzania italetwa kwa maridhiano na kuheshimiana.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.