MTANGAZAJI

DAR ES SALAAM:WANANCHI WA KISARAWE WASHIRIKI MDAHALO WA AJENDA YA WATOTO KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2015


Ndg Abel Mudo, mgombea wa udiwani kata ya Kisarawe kupitia CCM akichangia katika mdahalo wa ajenda ya watoto ambapo ulihusisha pia wakazi wa kata ya kisarawe
Baadhi ya wakazi ya kata wa kisarawe wakifuatilia kwa makini mdahalo wa ajenda ya watoto ambapo wa  ajenda ya watoto ullohusisha wagombea wa udiwani kupiitia vyama vya CCM na CHADEMA

Mmoja wa wananchi wa kata ya kisarawe akichangia katika mdahalo wa ajenda ya  watoto kuelekea uchaguzi mkuu  ambapo ulihusisha wanafunzi na wagombea  wa udiwani wa kata hiyo 


Mwanafunzi Amina Joka akichangia katika mdahalo wa ajenda ya watoto ambapo wanafunzi wa shule za Msingi  chanzige A ,chanzige B na kisarawe  na wagombea wa udiwani kupitia vyama vya ccm na chadema walishiriki

Ndg Abel Mudo ambaye ni mgombea wa Udiwani kupitia CCM akichangia katika mdahalo wa ajenda ya watoto kuelekea uchaguzi mkuu ambapo wanafunzi wa CHANZIGE ,na kisarawe 

Mmoja wa wanafunzi wa shule msingi Changize A akifuatilia kwa makini mdahalo wa ajenda ya watoto uliowahusisha wagombea wa udiwani wa vyama vya CHADEMA  na CCM 

Ndg .Baraka Musa, mgombea wa udiwani kata ya Kisarawe kupitia CHADEMA akichangia katika mdahalo huu uliowaohusisha wakazi wa kisarawe na wanafunzi

Picha za Wanafunzi ni za wanafunzi wa shule za msingi Chanzige A, Chanzige B na Kibasila zilizopo Kisarawe wakifuatilia kwa makini mdahalo huo.

Ndg .Baraka Musa, mgombea wa udiwani kata ya Kisarawe kupitia CHADEMA akichangia katika mdahalo huu uliowaohusisha wakazi wa kisarawe na wanafunzi
Ajenda ya watoto ilianzishwa na mashirika ya watoto Tanzania yakiongozwa na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa nia ya kuhakikisha maswala ya watoto na haki zao yanawakilishwa vyema katika serikali ya Tanzania.

Katika kuhakikisha kwamba Ajenda za watoto zinazungumzwa katika jamii Kipindi cha redio cha Walinde Watoto jana  kilifanya mdahalo uliowahusisha wagombea wa udiwani kata ya Kisarawe ambao ni Abel Mudo (CCM) na Baraka Musa (CHADEMA) na wakazi wa Kata ya Kisarawe ili kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabili watoto na mipango ya vyama vyao katika kutatua changamoto hizo.

Mdahalo huo uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ulihudhuriwa na wenyekiti wa vijiji, na vitongoji, walimu, maafisa ustawi wa jamii pamoja na wananchi wakazi wa Kata ya Kisarawe.

Mwanafunzi Amina Joka aliwataka wagombea udiwani hao pindi mmoja wapo atakapochaguliwa, wahakikishe wanajenga hosteli za wanafunzi kufikia kwani kwa sasa wanalazimika kusafiri umbali mrefu sana kwenda shule hali ambayo ni hatarishi kwani wanakutana na vishawishi vingi njiani. 

Unaweza kusikiliza kipindi cha Walinde Watoto mahali popote kupitia redio shiriki 19 ikiwemo TBC inayorusha matangazo hayo siku ya Jumamosi kuanzia saa nane mchana na pia kupitia tovuti ya www.walindewatoto.org

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.