MTANGAZAJI

NAIROBI:RAIS UHURU KENYATTA ALISIFU KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO




 

 


Rais Uhuru Kenyatta akisalimiana na Viongozi mbalimbali wa Kanisa la Waadventista Wa Sabato


 

Makamu wa Rais wa Kenya  William Ruto (wa pili toka kulia)akifafanua jambo

 

 

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amelisifu Kanisa la Waadventista Wa Sabato kwa namna linavyojihusisha katika  kuboresha maisha barani Afrika na akachangia dola 22,000 za kimarekani ambazo ni zaidi ya shilingi za kitanzania milioni 37 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la sayansi ya afya la Chuo Kikuu cha Afrika cha Kiadventista kilichopo Ong’ata Rongai,Nairobi nchini Kenya.

Akizungumza kwenye tukio hilo la kuchangia jengo hilo Rais huyo amesema kuwa anafurahishwa na kazi zinazofanywa na  kanisa hilo katika sekta za elimu na afya kupitia taasisi zake zilizoko nchini Kenya.

Katika changizo hilo Chuo Kikuu cha Afrika cha Waadventista kilichoko karibu na yalipo Makao Makuu ya Kanisa hilo kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati  kilifanikiwa kukusanya shilingi milioni 50 za Kenya kwa ajili ya ujenzi wa jengo jipya  la sayansi ya afya .

Tukio hilo pia lilihudhuriwa na viongozi waandamizi wa Serikali ya Kenya akiwemo Makamu wa Rais William Ruto  na pamoja na Kiongozi wa  Kanisa la Waadventista Wa Sabato katika Divisheni ya Afrika Mashariki na Kati Dr Brasious Ruguri

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.