MTANGAZAJI

MRADI WA VOLUNTEER TANZANIA WAJA





Mradi huu unaundwa ili kutatua matatizo makuu mawili:-

Kwanza: Ajira
Upande wa ajira ni kuwa vijana wengi wanamaliza shule wakiwa hawana ujuzi wa kutosha wa shughuli za uzalishaji hata zile ambazo wamesomea na kupata vyeti. Hivyo basi wanahitaji kupata fursa za kujishughulisha hususani wakisaidiwa na wale wenye uzoefu ili waweze kupata uzoefu utakaowawezesha kuwa imara katika kutafuta ajira katika soko gumu la ajira. 


Pili: Shughuli za kimaendeleo
Upande wa shughuli za kimaendeleo ni kwamba zipo shughuli nyingi za kimaendeleo zinakwama kwa sababu ya kukosa msukumo wa kiutendaji kwakuwa hawajapatikana watendaji wenye ujuzi unaotakiwa kufanya shughuli husika. Pia shughuli nyingi hukwama kwakuwa kuna rasilimali nyingine zinahitajika ila ni ngumu kupatikana kama vile fedha na vifaa kwakuwa wenye shughuli husika hawajawa na uwezo wa kutosha wa kifedha kununua vifaa husika, au hawajawa na ujuzi wa kutosha wa kiutendaji, kimuundo n.k katika kujizalishia rasilimali wanazozihitaji. 

Kwa maelezo zaidi tembelea ukurasa wetu wa facebook kwa kubofya hapa VoluteerTZ

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.