MTANGAZAJI

DEOGRATIUS KIDUDUYE HATUKO NAYE

Deogratius Kiduduye (wa tatu kutoka kulia) katika picha ya pamoja na waandishi wa habari toka nchi za Kusini mwa Afrika
Mwanahabari wa siku nyingi hapa nchini Deogratius Kiduduye (Kushoto) amefariki dunia kutokana na ugonjwa wa kisukari kwa mujibu wa matangazo yaliyotolewa na Radio Free Afrika,Mwanza ambako alikuwa miongoni mwa watangazaji wa kwanza walioanzisha redio hiyo hapaTanzania

Mpaka mauti yanamkuta Kiduduye alikuwa ni mtangazaji katika kituo cha Radio Uhuru cha jijini Dar es salaam,nitaendelea kumkumbuka sana mwanahabari huyu kwa ushauri aliokuwa akinipa hasa kutokana na masuala ya utangazaji.

June 2007 Mimi na Marehemu Kiduduye tulibahatika kuhudhuria mafunzo ya wiki mbili ya uandishi wa habari huko Lusaka,Zambia.Mafunzo hayo yaliyoendeshwa na NSJ ambayo yalihusu "Communication for Social Change"na kufanyika katika Hotel ya Longacres yaliwakutanisha waandishi wa habari 14 toka nchi za Tanzania,Zambia,Malawi,Lesotho,Botswana,DRC,Msumbiji na Zimbabwe. Nakumbuka tukiwa Zambia huko alininiuliza swali moja "je unafahamu Tanzania ilivyouzwa? na akanionesha email aliyokuwa ametumiwa iliyokuwa na orodha ya majina ya watu "walichota" pesa za walalahoi ambao miongoni mwao hivi sasa wanatuhumiwa kuwa ni MAFISADI. Huyo ndo Kiduduye ambaye amelala usingizi wa mauti.

1 comment

moses kiduduye said...

I LOVE YOU DAD MAY YOUR SOUL REST IN PEACE.

Mtazamo News . Powered by Blogger.