MTANGAZAJI

TATHIMINI YA NDOA!!!


JE UNAMTHAMINI MWENZAKO UNAVYOTHAMINI
MARA NGAPI UMEFANYA HAYA KWA MME/MKE WAKO

Mara ngapi umeamka asubuhi ukamsalimia mme/mke wako
Mara ngapi umemu-HUG mme/mke wako na kumbusu
Mara ngapi umesema samahani ulipomkosea mme/mke wako
Mara ngapi umeoga na mme/mkeo
Mara ngapi umekula chakula na mme/mkeo
Mara ngapi umem-SMS mume/mke msg za mapenzi
Mara ngapi umemvumilia mme/mke wako alipokukosea?
Mara ngapi umekataa jambo kwa mme/mke wako huku umefanya?

WEKA NDIYO/HAPANA

Una mazoea ya kumkumbatia mme/mke wakati wa kulala
Una mazoea ya kumwambia mme/mke wako hisia zako kimapenzi?
Una mazoea ya kumficha mme/mke mambo yako
Una mazoea ya kumthamini mme/mke wako mbele za watu
Una mazoea ya kumsimulia vema mme/mke wako kwa ndugu zako
Una mazoea ya kumuuliza mme/mke wako kuhusu maendeleo yenu
Una mazoea ya kumtukana na kumgombeza mme/mke wako?
Una mazoea ya kukaa kimya unapokutana na mme/mke wakati wa Sex
Una mazoea ya kumwambia mme/mke wako nakupenda kumbe humpendi?

Unadhani ukipewa nafasi nyingine ya uchaguzi utamchagua mme/mke uliyenaye?
Unadhani mambo unayomfanyia mme/mke kwa siri hatajua?
Unadhani kutoka nje ya ndoa kutakupa furaha kuliko ndani ya ndoa?

Umewahi kumwambia asiye mume/mke wako kuwa unampenda
Umewahi kumsaliti mme/mke kwa namna yoyote ikiwamo kutoka nje ya ndoa
Umewahi kumdanganya mme/mke wako kwa namna yoyote ile

Kuna mambo mengi zaidi ya haya, ila ukweli ni kwamba majibu yako uliyotoa
kwenye kila swali ndiyo jibu la ndoa yako.

NDOA ni njema sana, ila waliomo wanaiendesha ndoa bila kumshirikisha
Mungu aliyewapa ndoa, Wana ndoa hawaweki mambo yao kwa Mungu hadi
litokee tatizo, Kumbuka siku ulipofunga ndoa Mungu ndiyo alikuwa shahidi
mwaminifu, na mwanzilishi wa ndoa yenu, lakini shida inapotokea mnasahau
kumwambia Mungu ili awape njia ya kutokea.
Mungu anasema: KILA JARIBU
LITAKALO WAPATA NITAWAPATA MLANGO WA KUTOKEA.

Ngao Kuu ya Ndoa ni upendo, Uaminifu na uvumilivu

Kumbukeni kusali kila mara mkutanapo ili shetani asije akawatumia kuivunja ndoa yenu
Kumbukeni hakuna jambo linalomshinda Mungu

1 comment

Esther said...

MUME WANGU jina: anaitwa TITUS MATHIAS TOSSY ALIKUWA VERY FERMACY IN ARUSHA BARAKA TELE BASI ALIFANYA FUJO SANA KATIKA NDOA YETU. MACHONI MWAMINIFU KUMBE SIYO. LEO ANAISHI NA CHANGUDOA NA WAMEZAA MTOTO WA KIKE, YEYE KWAO WALIMWAMBIA ANIFUKUZE AOE ILI AZAE WA KIUME MUNGU NAE HUYO KWAKE, BADO HASALI KABISA. MWANZO WA UGOMVI NILIMUELEZA PASTOR SOKA NJIRO SDA KUWA MWENZIO AMEPOTOKA HAWAKUJALI, BASI AKAWA ANACHUKUA WANAFUNZI WAKE HADI NDIO MWANAFUNZI ANAISHI NAE NA KUZAA MTOTO WA KIKE.

OMBI. WASABATO NA UZINZI BILA HOFU YA MUNGU wanatuyumbisha katkika ndoa.

WASABATO CHANGAMKENI TATIZO LOLOTE LIKITOKEA KWELI WACHUNGAJI NJIRO NAO WAMECHANGIA UVUNJIKAJI WA NDOA YANGU KWANI walimuamini sana, mimi niliwaeleza yote aliyowaeleza ni uongo haya leo ukweli hadharani, yuko wapi MWALIMU TITUS MATHIAS TOSSY ALIYEKUWA MWALIMU UNIVERSITY OF ARUSHA?CHANGAMKENI KUOKOA KONDOO KWANI WATOTO WETU SIJUI WATAMUABUDU NANI? MBINGU ZIINGILIE KATI JUU YA TITUS MATHIAS TOSSY. ALIKUWA MWINJILISTI NA MUHUBIRI SANA. PESA ZIMEMCHANGANYA LEO HANA PESA ANAWEZA AKAJIRUDI - TUOMBEANE. SERIOUS

Mtazamo News . Powered by Blogger.