MTANGAZAJI

ALIYEWAHI KUWA KIONGOZI WA WA ADVENTISTA AFARIKI

 



Asubuhi ya  Julai 23, 2022, Daniel R. Jackson, aliyewahi kuwa Mwenyekiti  wa Kanisa la Wa Adventista wa Sabato katika Divisheni ya  Amerika Kaskazini (NAD) alifariki dunia baada ya miezi kadhaa ya kuugua saratani. Alikuwa na umri wa miaka 73.

Jackson, ambaye alitumikia Kanisa la Wa Adventista wa Sabato kwa miaka 49, alistaafu Julai 2020 baada ya kuhudumu katika nafasi ya Mwenyekiti  wa Divisheni ya  Amerika Kaskazini (NAD) kwa muongo mmoja.

Divisheni ya Amerika ya Kaskazini yenye makao yake makuu nchini Marekani ilianzishwa rasmi mwaka 1913 na kupangwa tena mwaka 2012,miongoni mwa nchi zilizoko katika eneo hilo ni Marekani na Canada,Divisheni ambayo kwa mujibu wa takwimu za Juni 30,2021 ina makanisa 5,650,Wa Adventista 1,267,711 kati ya wakaazi  wapatao 370,959,000

Akiwa mwenyekiti ,Jackson alishiriki kikamilifu katika Divisheni hiyo wakati wa huduma yake ya miaka 10 katika kitengo hicho, ikiwemo  kujengwa kwa Chama cha Wachungaji wa NAD; kuundwa kwa mpango mkakati wa utume na kuongezwa kwa utume wa  Guam-Micronesia, Chuo Kikuu cha Oakwood, Jumuiya ya Nyumba ya Uchapishaji ya Pacific, AdventSource, na Huduma za Utunzaji wa Kumbukumbu za Waumini wenye ulemavu wa kutoona.

Pia alihusika katika maamuzi ya Ofisi za Divisheni kuhamia kwenye makao yake makuu huko Columbia, Maryland, mnamo 2017, taarifa za matoleo zikitolewa kwa ukamilifu,kuanzishwa kwa makanisa karibu 1,000 na watu 300,000 wakibatizwa na kuimarika kwa utume wa vyombo vya habari ikiwemo vilivyoko katika eneo hilo ikiwemo Breath of Life, Faith for Today, It Is Written, Escrito Está, Jesus 101, La Voz de la Esperanza, Lifetalk Radio,Sauti ya Unabii na matumizi ya Kidigitali katika utume wa Kanisa hilo.

Jackson alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Divisheni ya Amerika Kaskazini Juni 28, 2010, na wajumbe wa kanisa hilo duniani  katika Kikao cha Konferensi Kuu huko Atlanta, Georgia, na kuchaguliwa tena kwa nafasi hiyo  Julai 6, 2015, katika Kikao cha 60 cha Konferensi Kuu kilichofanyika San Antonio, Texas. Kikao cha Konferensi Kuu ndicho chombo cha juu zaidi cha uongozi katika Kanisa la Waadventista Wa Sabato Duniani.

Jackson mzaliwa wa Canada japo ilihudumu miaka mitano katika Divisheni ya Kusini mwa Asia, aliishi na kuhudumu katika Divisheni ya Amerika Kaskazini.Alikuwa mhitimu wa Chuo cha Unioni ya Canada (sasa Chuo Kikuu cha Burman) na Chuo Kikuu cha Andrews, ambako alihitimu Shahada ya Udhamili katika Dini na  Thiolojia, Jackson alikuwa mmoja wa waandishi wa kitabu cha Becoming a Mission-Driven Church.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.