MTANGAZAJI

RAIS SAMIA AANDIKA HISTORIA MPYA

 

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Samia Suluhu Hassan ameweka historia mpya kwa kuwa Rais na Amiri Jeshi mwanamke wa kwanza toka Tanzania ilipopata Uhuru wake mwaka 1961 kuhutubia Mkutano  wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

 Rais Samia aliyezaliwa Januari 27, 1960 (kwa mujibu wa mtandao wa wikipedia)  aliingia madarakani mwaka huu baada ya Kifo cha aliyekuwa Rais wa awamu ya tano nchini Tanzania Hayati John Pombe Magufuli aliyefariki mwezi Machi 2021. 

Rais Samia yuko nchini Marekani na amehutubia  mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, katika Ukumbi wa Umoja wa Mataifa Jijini New York,Marekani Septemba 23,2021. Rais huyo ameongozana na Waziri wa Mambo ya Nje  na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.