MTANGAZAJI

WATANZANIA WATAKIWA KUNUNUA BIDHAA ZENYE ALAMA YA UBORA

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS)  Dkt Yusuph Ngenya ametoa wito kwa  watanzania kutonunua bidhaa yoyote bila kuhakikisha kwamba ina alama ya ubora kwa bidhaa zinazozalishwa nchini.

Ngenya aliyasema hayo eneo la Mwahako Jijini Tanga katika  maonyesho ya nane ya Biashara ambapo alisema hatua hiyo itasaidia kuwaondolea hasara ambazo wamekuwa wakikumbana nazo kutokana na bidhaa wanazonunua kutokuwa na ubora unaotakiwa.

Alisema bidhaa zimekuwa na athari nyingi katika matumizi ya binadamu hivyo ni muhimu watanzania kutambua kwamba wanaponunua bidhaa wanapaswa kuzikagua na kuona kama zina ubora unaotakiwa ili kuweza kuepukana na majanga ambayo yanaweza kuwakuta kutokana na bidhaa  feki.

“Lakini hata katika operesheni zetu ambazo tumekuwa tukizifanya tunagundua  bidhaa gani ambazo zinaingizwa kwenye masoko na hazina ubora ikiwemo bidhaa za ujenzi ,vifaa vya umeme vingi vinakuja feki hivyo tujitahidi kuvitambua na kuviondoa kwenye soko kwani mfano vifaa vya umeme madhara yake vinaweza kushika moto na kuweza kuharibu mali”Alisema Mkurugenzi huyo wa TBS

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.