MTANGAZAJI

TASAC KUNUNUA BOTI KUZUIA VITENDO VYA UCHAFUZI WA MAZINGIRA BAHARINI

 Shirika la Wakala wa Meli Tanzania (TASAC) kupitia Meneja wake Nelson Mlali amesema shirika hilo lipo kwenye utaratibu wa manunuzi ya boti ambayo itapita maeneo mbalimbali kuelimisha jamii ikiwa ni mkakati wa kuzuia vitendo vya uchafuzi wa mazingira kwenye bahari.

Mlali aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Tanga kwenye maonyesho ya biashara yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwahako Jijini hapa ambapo alisema kabla ya mwaka huu kwisha itapatikana ili waweze kushirikiana na taasisi nyengine.

Alisema taasisi ambazo watashirikiana nazo ni zile ambazo zinaangalia maeneo hayo kiusalama wa mazingira na pia kiusalama wa nchi kwa sababu bandari ni mipaka ya kimataifa.

Alisema kwa Tanzania uchafuzi wa mazingira kwenye pwani yao sio mkubwa kama zilivyo nchi nyengine huku akibaini changamoto zinazowakabili ni wananchi kutokufahamu shirika hilo na shughuli wanazofanya kwa sababu bado ni changa hivyo wapo kwenye utaratibu wa kutoa elimu kwa wananchi.

“Elimu hiyo itakuwa ni kuhusu biashara za kimataifa kupitia njia za maji zinazofanyika kwa hivyo tumekuwa tukifanya mikutano mbalimbali ya kuwapa uelewa mkubwa”Alisema
 
Alisema uingiaji wa meli nchini umeongezeka hasa kwa sababu ya madhara yaliyotokana na COVID 19 kwa nchi nyengine ambazo walikuwa wameweka vizuizi lakini kwa hapa nchini hatukujaweka na hivyo kuruhdu meli kuja kuleta shehena na kubadilisha mabaharia.

“Meli kutoka Dunia nzima zimekuwa zikiingia kwa mfano za mafuta zinazotoka ukanda wa Huba zinaleta mafuta ikiwemo Kuiwati,Saudi Arabia na nchi nyengine nyingi..,Meli za ngano kutoka Ulaya Mashariki na nyengine dunia nzima”Alisema Hata hivyo alitoa wito kwa wafanyabiashara wazingatia masuala ya usalama wanapotumia njia za usafiri wa majini na wanapopanda vyombo na wanaposafirisha mizigo huku akiwataka wamiliki wa vyombo wafuate utaratibu.



 

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.