MTANGAZAJI

JKT TANZANIA YASITISHA MAFUNZO

Kaimu Mkuu wa Utawala wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Kanali Hassan Mabena akieleza
kwa waandishi wa habari kuhusu kusitishwa kwa mafunzo ya kundi la kujitolea kwa mwaka
2020/2021 wakati wa mkutano uliofanyika makao makuu ya Jeshi hilo wilayani Chamwino
mkoani Dodoma Januari 19, 2021, Mafunzo hayo yalipangwa kuanza hivi karibuni katika
makambi mbalimbali ya JKT.



 Jeshi la Kujenga Taifa nchini Tanzania (JKT) limesitisha kwa muda Mafunzo kwa kundi la kujitolea kwa mwaka 2020/2021 kwa vijana waliokuwa wamechaguliwa kushiriki mafunzo hayo yaliyotarajiwa kuanza hivi karibuni nchini kote.

 Kaimu Mkuu wa Utawala, Kanali Hassan Mabena amewaambia waandishi wa habari  kwenye  mkutano wake na waandishi hao uliofanyika Makao Makuu ya Jeshi hilo wilayani Chamwino mkoani Dodoma.


“Kutokana na kusitishwa kwa mafunzo hayo, JKT inawataka vijana wote ambao walichaguliwa na kuripoti makambini kwa ajili ya kuhudhuria mafunzo ya JKT kwa kujitolea warejee majumbani kwao” alisisitiza Kanali Mabena.

Kanali Mabena amewataka vijana ambao waliokuwa hahawajaripoti wasiende kuripoti katika makambi waliyopangiwa mpaka watakapotangaziwa tena.


Jeshi la Kujenga Taifa limekuwa likiwajengea vijana uwezo wa kujiajiri kupitia stadi za maisha wanazopata katika mafunzo yanayotolewa kwa mujibu wa sheria na yale ya vijana kujitolea, hivyo kuwawezesha kuwa wazalendo wanaoshiriki kikamilifu katika ujenzi wa Taifa la Tanzania.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.