MTANGAZAJI

HOSPITALI YA UHURU YAANZA KUTOA HUDUMA

 

Mwonekano wa sasa wa  Jengo la Hospitali ya Uhuru iliyoko Dodoma ,Tanzania


Katibu wa kuratibu shughuli za Serikali kuhamia Dodoma Meshack
Bandawe akikagua vifaa mbalimbali vilivyopo katika hospitali ya Uhuru
ambayo imekamilika na kuanza kutoa huduma kwa wagonjwa wa nje.

Hospitali ya Uhuru inayojengwa kwa gharama za bilioni 3.9 imeanza  kutoa huduma kwa wagonjwa wa nje.

 

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino Dkt. Dkt.Eusebius Kessy ametoa taarifa hiyo alipokuwa akiongea  na waandishi wa habari wakati wa ukaguzi wa hospitali hiyo.

 

“Hospitali yetu imeanza kutoa huduma tangia tarehe 21 Desemba 2020 na mpaka sasa imeshahudumia wateja takribani 300”amesema Dkt Kessy

 

Ameongeza kuwa ujenzi wa hospitali hiyo ni ukombozi mkubwa kwa wananchi wa chamwino na maeneo ya karibu na kusema kuwa watahahakisha kwamba huduma zinakuwa bora kama ilivyokusudiwa

 

Dkt Kessy amesema kuwa hospitali iyo inatoa huduma kwa wagonjwa wenye     Bima ya afya ya Taifa NHIF na Mfuko wa afya ya jamii (CHF) na pia wale ambao hawana Bima ya afya.

 

Akizungumzia huduma zinazotolewa kwa sasa Dkt.Kessy amesema kwa sasa huduma za maabara,clinic za macho na meno,mionzi ,clinic za mama na mtoto na huduma za wagonjwa wa nje (OPD).

 

Kwa upande wake Katibu wa kuratibu shughuli za Serikali kuhamia Dodoma Meshack Bandawe ambae alifanya ziara maalum kukagua imaendeleo ya Hospitali hiyo amesema kuwa kuwa ujenzi wa hospitali hiyo umekamilika kwa asilimia 99.8.

 

Pamoja na hayo amesema mifumo ya maji na umeme na miundombinu mbalimbali imekamilika pamoja na vifaa tiba vya Utra sound, X-ray,ECG na baadhi ya samani ambavyo vimeshawasili hospitali hapo.

 

Amesema siku ya sherehe za mapinduzi ya Zanzibar kulifanyika uchangiaji wa damu salama na kufanikiwa kupata unit 48 za damu.

 

Ujenzi wa Hospitali ya Chamwino ni agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwamba Fedha  zilizotengwa kwa ajili ya sherehe ya miaka 57 ya Uhuru wa Tanzania bara za tarehe 9 Disemba 2018 zitumike kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Chamwino.

 

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.