MTANGAZAJI

WADAU WAJADILI UTEKELEZAJI WA MKAKATI WA KITAIFA KUTOKOMEZA MAUAJI DHIDI YA WAZEE TANZANIA

Picha ya Pamoja ya washiriki wa mkutano wa kujadili utekelezaji wa mkakati wa kutokomeza mauaji ya wazee uliofanyika jijini Dodoma. Waliokaa kutoka kulia ni Mwenyekiti wa wazee Mkoa wa Shinyanga Mzee Sengerema, Kamishna wa Ustawi wa Jamii Dkt. Naftali Ng’ondi, Mwenyekiti wa Mtandao wa mashirika yanayotetea wazee nchini Cotilda Isidory, Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya – Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Sayi Magessa na mwakilishi kutoka Idara ya Operesheni na Mafunzo Jeshi la Polisi Boniphace Isaack.


Imeelezwa kuwa Idadi ya Mauaji ya wazee imepungua nchini Tanzania kutoka 557 kwa mwaka 2014 hadi wazee 74 mwaka 2019 na kuwa hadi mwaka huu idadi ya wanauawa kwa sababu mbalimbali ni chini ya wazee 10 mwaka mwaka.

Taarifa hiyo imetolewa  jijini Dodoma na Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii nchini Tanzania Sayi Magesa kwa wadau mbalimbali wanaoshughulika na masuala ya wazee nchini Tanzania waliokutana kujadili hatua iliyofikiwa ya utekelezaji wa mkakati wa Kimataifa wa Kutokomeza mauaji dhidi ya wazee 

 



Ameeleza kuwa Mkakati huo umesaidia sana kupunguza kutoka 557 mwaka 2014 hadi 74 mwaka 2019 lakini hadi sasa idadi inazidi kupungua hadi kufikia mmoja hadi tisa, kipindi kama hiki cha uchaguzi hali ilikuwa mbaya pia hata kwa walemavu kutokana na Imani potofu tu

Mkutano huo unalenga kuangalia mafanikio, changamoto na malengo zaidi ya baadaye ili kufanikisha kutokomeza kabisa mauaji ya wazee.

 Ripoti ya kituo cha Sheria na Haki za Binadamu nchini Tanzania  ya mwaka 2009 ilionyesha kuwa wanawake wazee 2,583 walikuwa wameuawa katika mikoa minane ikiwa ni wastani wa mauaji 517 kila mwaka.

Kamishna wa Ustawi wa Jamii nchini nchini Tanzania Dkt. Naftali Ngóndi ametoa rai kwa vyombo vinavyohusika na upelelezi pamoja na hukumu kuhusu mauaji ya wazee kusaidia ili jamii itambue kuwa jambo hili ni kosa kwani wazee wana haki ya kuishi na kufurahia maisha.

Meneja wa Programu Haki kwa Wazee na ushirikiano wa Wadau kutoka Shirika la HelpAge International Joseph Mbasha amesema kwa ushirikiano na jitihada za wadau, nchi Tanzania  unakwenda vizuri katika kutokomeza mauaji ya wazee kwani takwimu zimepungua sana pamoja na kuwa barani Afrika nchi nyingi zilikumbwa na janga hilo kutokana na Imani potofu.

Mmoja wa Wazee walioshiriki mkutano huo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mtandao wa mashirika yanayotetea Wazee nchini Bi. Cotilda Isidory amesema tangu Serikali kupitia vyombo vyake mbalimbali iingilie kati suala la mauaji ya wazee, hivi sasa yamepungua kwa kiasi kikubwa kwani hapo kabla wameuawa wengi hali iliyokuwa inawatisha wazee hao.

Katika mkutano huo, washiriki walibainisha kuwa Serikali katika ngazi zote ikishirikiana na wadau ikiwemo vyombo vya Habari, kwa Pamoja walifanya jitihada kubwa kuhakikisha mauaji ya wazee yanakwisha.

 

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.