MTANGAZAJI

KONGAMANO LA WANAUME WAADVENTISTA TEXAS LAFANA






Wanaume Waadventista wapatao 600 wanaotoka katika makanisa ya Konferensi ya Texas  wamehudhuria Kongamano la mwaka lililopewa kauli mbiu ya UNBROKEN lengo likiwa  kujifunza na kubadilisha uzoefu wa mafaniko na matatizo ya Kiroho,Jamii na Taifa wanayokumbana nayo wanaume Waadventista nchini Marekani.

Katika Hotuba yake kwenye Kongamano hilo lililofanyika ndani ya Ukumbi wa
Mikutano wa Kanisa la Waadventista la Houston Central na kurushwa mbashara kwa Youtube na Facebook,Mhubiri wa Kimataifa na Rais wa Amazing Facts Mchungaji Doug Batchelor aliwataka wanaume hao kuwa na tabia ya kusameheana katika familia,jamii na Kanisa kwa ujumla kwa kuwa kutofanya hivyo ni  kuwa mwanamme aliyevunjika katika maisha ya Kiroho na kutokuwa na tabia ya Kristo maishani.

Akieleza uzoefu wa Maisha yake Batchelor alisema alizaliwa kwenye familia yenye ukwasi wa mali lakini kutokana na tabia ya Baba yake ya ulevi ilisababisha  hatimaye akajiingiza katika masuala ya ulevi,utumiaji wa madawa ya kulevya,uhalifu na kuishi mapangoni lakini Yesu alimwita na sasa ni mhubiri wa Kimataifa.

Rais  wa US Dream Academy,Mwimbaji wa Kimataifa na Mchungaji Wintley Phipps  aliwataka wanaume kujenga tabia ya kutotumia mabavu kwenye kila jambo katika maisha yao  ya kila siku bali wawe watu wanaokubali kusaidiwa katika mambo ambayo hawawezi kuyatenda.

Mada mbalimbali zilizotolewa na kujadiliwa ni masuala ya mahusiano ya wanaume na wenza wao,matatizo ya afya na jinsi ya kukabilina nayo hasa ulaji wa vyakula bora na mitindo ya maisha inavyosaidia kuboresha afya ya mwili na akili huku baadhi ya wanaume wakitoa ushuhuda wa namna walivyo nyanyaswa katika famili wakati wakiwa wadogo.

Kongamano hilo lililohudumiwa na Waimba maarufu nchini Marekani A'Men Quartet,Neville Peter na Mark Bunney, lililohitimishwa kwa huduma ya meza ya BWANA huku likiwatambua wanaume wa Waadventista waliostaafu kutumikia Jeshi la Marekani zaidi ya 20 waliohudhuria kwa kuwapa medali za kutambua mchango wao katika jamii.

No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.