MTANGAZAJI

SERIKALI YA TANZANIA YAPOKEA GAWIO LA SH. BILIONI MOJA KUTOKA TPB BANK


Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Phillip Mpango  akipokea mfano wa Hundi yenye thamani ya Shilingi Bilioni Moja kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya TPB, Dkt. Edmund Mdolwa  katika  hafla ya kupokea gawio hilo  jijini Dodoma. Benki ya Posta imetoa gawio hilo ikiwa ni faida iliyopatikamna mwaka 2018.
Serikali  ya Tanzania imepokea gawio la Shilingi Bilioni Moja kutoka Benki ya Posta Tanzania (TPB) linalotokana na faida ya uwekezaji wake wa asilimia 83 ya hisa  katika Benki hiyo katika mwaka wa fedha 2018/19.

Hafla ya makabidhiano ya Hundi kifani ya gawio hilo imefanyika jijini Dodoma, kati ya Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) ambaye alipokea kwa niaba ya Serikali, na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki hiyo Dkt. Edmund Mndolwa.

Akizungumza katika hafla hiyo Dkt. Mpango aliipongeza Benki hiyo kwa kutoa gawio kwa Serikali, na kuahidi kuwa fedha hizo zitatumika katika shughuli mbalimbali za maendeleo nchini huku akiitaka Benki hiyo kuongeza wigo wa utoaji huduma ili kuwafikia wananchi hususani waishio vijijini pamoja na kutoa elimu kwa wananchi hao kuhusu umuhimu wa  kuweka akiba, kukopa sambamba na kurejesha mikopo kwa wakati.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TPB Dkt. Edmund Mndolwa alisema kuwa gawio hilo ni sehemu ya faida ya Sh. Bilioni 17.2 kabla ya kodi ambayo Benki yake imeipata katika mwaka wa fedha 2018/19. Pia ameeleza kuwa Benki hiyo itaendelea kutoa huduma bora ili kukidhi mahitaji ya wanahisa wake na wananchi kwa ujumla.


No comments

Mtazamo News . Powered by Blogger.